Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 7 Sitting 19 Water and Irrigation Wizara ya Maji 167 2022-05-10

Name

Anton Albert Mwantona

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Rungwe

Primary Question

MHE. ANTON A. MWANTONA aliuliza: -

Je, ni lini mradi wa maji wa Tukuyu utakamilika?

Name

Maryprisca Winfred Mahundi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAJI alijibu: -

Mheshimiwa Spika, ahsante. Kwa niaba ya Waziri wa Wizara ya Maji naomba kujibu swali la Mheshimiwa Anton Albert Mwantona Mbunge wa Rungwe, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, katika mwaka wa fedha 2021/2022, Serikali imeendelea kutekeleza mradi wa maji wa Tukuyu Mjini ambapo kazi zilizopangwa ni pamoja na uhifadhi wa chanzo, ulazaji wa bomba kuu Kilometa 9.5, ulazaji wa mabomba ya usambazaji Kilometa 20 na ujenzi wa tenki la ukumbwa wa lita 1,500,000.

Mheshimiwa Spika, hadi sasa kazi zilizofanyika ni pamoja na uboreshaji wa chanzo cha maji na ulazaji wa bomba kuu lenye urefu wa Kilometa tatu.

Mheshimiwa Spika, utekelezaji wa mradi huo ulianza mwezi Septemba, 2021 na unatarajiwa kukamilika ifikapo mwezi Machi, 2023. Mradi huo utasaidia kuboresha huduma ya upatikanaji wa maji katika Mji wa Tukuyu kutoka asilimia 67 na kufika asilimia 90.