Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Hamida Mohamedi Abdallah

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Lindi Mjini

Primary Question

MHE. HAMIDA M. ABDALLAH aliuliza:- Je, ni lini Serikali itajenga Chuo Kikuu cha Uvuvi na Usafirishaji baharini katika eneo la Kikwetu - Lindi ambapo tayari Ekari 150 zimetengwa kwa ajili ya kazi hiyo?

Supplementary Question 1

MHE. HAMIDA M. ABDALLAH: Mheshimiwa Spika, ahsante sana. Ninamshukuru Mheshimiwa Waziri kwa majibu ya Serikali ambayo yameonesha matumaini sasa ya kuanza mchakato wa ujenzi wa Chuo cha Usafiri na Usafirishaji pale Kikwetu.

Mheshimiwa Spika, Halmashauri ya Manispaa ya Lindi tumetoa Hekari 125 bure kwa Ndugu zetu hawa wa NIT, lakini hekari 150 kwa Ndugu zetu wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam kwa ajili ya ujenzi wa Chuo cha Kilimo pale Lindi Mjini, sasa ni miaka mitatu, ningependa kuuliza maswali mawili ya nyongeza kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, Je, ni lini sasa Serikali itawawezesha ndugu zetu wa NIT kuwapatia fedha kwa ajili ya kuharakisha ujenzi wa chuo hiki cha Usafiri na Usafirishaji? (Makofi)

Mheshimiwa Spika, swali la pili tunategemea kwamba chuo cha Kilimo Kampasi ya Lindi tungependa sasa kuongeza Kitivo cha Uvuvi na masuala ya kilimo cha Mwani kutoa fursa ya ajira kwa vijana na wananchi wa maeneo hayo ya Lindi na Mtwara. Ahsante. (Makofi)

Name

Abdallah Hamis Ulega

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mkuranga

Answer

NAIBU WAZIRI WA MIFUGO NA UVUVI: Mheshimiwa Spika, nashukuru sana kwa maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Hamida Abdallah Mbunge wa Lindi Mjini. Mbunge huyu ni katika Wabunge wafuatiliaji sana wa masuala ya Wavuvi

Mheshimiwa Spika, swali lake la kwanza ni hili la lini watapewa fedha NIT. Nafikiri ni wakati mzuri ameuliza swali hili kwa sababu ni kipindi ambapo Serikali tupo katika kuwasilisha bajeti hapa Bungeni na kwa hivyo chuo cha NIT ni chuo cha Serikali na kipo katika hodhi ya Wizara zetu na hili litajibiwa wakati Wizara husika itakapokuwa ina wasilisha bajeti yake hapa.

Mheshimiwa Spika, jambo la pili ni juu ya jambo la Kitivo ha Kilimo kuhusianisha na course za mifugo na uvuvi. Wazo na fikra aliyoitoa Mheshimiwa Hamida ni nzuri na mimi naomba niichukue kwa niaba ya Serikali ya Serikali na kwa hivyo basi tutaipeleka kwa wenzetu wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam kama ilivyo desturi waweze kuunganisha fani hizi nazo ziweze kutolewa pale pindi chuo kitakapokuwa tayari. (Makofi)