Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 7 Sitting 19 Livestock , Fisheries, Agriculture, Food Security and Cooperatives Waziri wa Mifugo na Uvuvi 166 2022-05-10

Name

Hamida Mohamedi Abdallah

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Lindi Mjini

Primary Question

MHE. HAMIDA M. ABDALLAH aliuliza:-

Je, ni lini Serikali itajenga Chuo Kikuu cha Uvuvi na Usafirishaji baharini katika eneo la Kikwetu - Lindi ambapo tayari Ekari 150 zimetengwa kwa ajili ya kazi hiyo?

Name

Abdallah Hamis Ulega

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mkuranga

Answer

NAIBU WAZIRI WA MIFUGO NA UVUVI alijibu: -

Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Mifugo na Uvuvi, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Hamida Mohamed Abdallah, Mbunge wa Lindi Mjini, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, Wizara ya Mifugo na Uvuvi haina mpango wa kujenga Chuo Kikuu cha Uvuvi katika eneo la Kikwetu Lindi Mjini. Hata hivyo, Serikali kupitia Chuo cha Taifa cha Usafirishaji kwa maana ya NIT imepewa eneo lenye ukubwa wa ekari 125 lililopo Kikwetu Lindi. Eneo hilo ambalo tayari NIT imekamilisha taratibu za kumiliki, litatumika kwa ajili ya ujenzi wa Kampasi ya Lindi ya Chuo cha Taifa cha Usafirishaji ambacho kitatoa kozi katika ngazi ya Astashahada, Stashahada na Shahada katika fani mbalimbali za usafirishaji na uchukuzi ikiwemo Utengenezaji wa meli, uendeshaji wa vyombo vya majini na huduma za bandari.

Mheshimiwa Spika, kwa mwaka 2022/2023 kazi zitakazofanyika katika eneo hilo ni kuandaa mpango kabambe wa matumizi bora ya ardhi katika eneo hilo. Sambamba na maelezo hayo, napenda kulijulisha Bunge lako Tukufu kwamba, Serikali kupitia Chuo Kikuu cha Dar es Salaam inatarajia kujenga Kitivo cha Kilimo katika Halmashauri ya Lindi Mjini ambapo tayari wameomba kupatiwa hekta 500.

Mipango ya maandalizi ya ujenzi wa chuo hicho inaendelea kwa ushirikiano kati ya Mkoa wa Lindi, Halmashauri ya Lindi Mjini na Chuo Kikuu cha Dar es Salaam.