Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Dr. Raphael Masunga Chegeni

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Busega

Primary Question

MHE. DKT. RAPHAEL M. CHEGENI (K.n.y MHE. SALOME W. MAKAMBA) aliuliza:- Wafanyakazi wa migodi ya uchimbaji wa madini hufukuzwa kazi kiholela bila kulipwa fidia stahiki kutokana na ulemavu na magonjwa yanayosababishwa na vitendea kazi hatarishi wakati wakiwa kazini. (a) Je, Serikali iko tayari kuzuia kuingizwa nchini vitendea kazi hatarishi na kufunga migodi ambayo ina wahanga wengi na ulemavu na magonjwa yatokanayo na shughuli za uchimbaji madini? (b) Je, ni lini Serikali itaanza kutumia Sheria ya Fidia Na. 20 ya mwaka 2008 ili wafanyakazi wa migodini walipwe fidia stahiki wanapopata ulemavu au magonjwa wanapokuwa kazini badala ya Sheria ya Fidia ya mwaka 2002? na (c) Je, Serikali inatoa tamko gani kwa waajiri wanaowatelekeza wafanyakazi waliopata ulemavu wakiwa kazini na kukataa kuendelea kulipa gharama za matibabu yao?

Supplementary Question 1

MHE. DKT. RAPHAEL M. CHEGENI: Mheshimiwa Naibu Spika, pamoja na majibu mazuri ya Mheshimiwa Naibu Waziri, napenda kuuliza swali dogo la nyongeza.
Kwa kuwa waathirika wengi wa ulemavu, kama alivyosema Mheshimiwa Amina Mollel, katika migodi hii wanapata matatizo mengi sana wanapojikuta kwamba wanapoteza viungo vyao au wanapata ulemavu wakiwa kazini; na kwa kuwa waajiri wengi na hasa migodi hii wamekuwa hawalipi fidia wafanyakazi hawa wanaopata matatizo, na Sheria Namba 20 ambayo inaanza kutumika kuanzia mwezi ujao Mheshimiwa Naibu Waziri amesema kwamba ndiyo itaanza kushughulikia masuala haya.
Je, kwa wale waajiri ambao wamekaidi kwa muda mrefu, Serikali inatoa tamko gani ili kusudi wafanyakazi hawa ambao wameumia wakiwa kazini waweze kupata fidia zao?

Name

Anthony Peter Mavunde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Dodoma mjini

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA WAZIRI MKUU, KAZI, VIJANA NA AJIRA: Mheshimiwa Naibu Spika, katika swali lake la msingi Mheshimiwa Mbunge anauliza Serikali inachukua hatua gani au inatoa tamko gani kwa waajiri wote ambao wanakaidi kuwafidia wafanyakazi ambao wameathirika kutokana na magonjwa yanayotokana na kazi.
Mheshimiwa Naibu Spika, kama nilivyosema katika majibu yangu ya msingi, Sheria Namba Nane ya mwaka 2008 ambayo imeunda Mfuko wa Fidia kwa wafanyakazi kupitia kifungu cha tano cha sheria hiyo itaanza kufanya kazi tarehe 1 Julai, 2016.
Mheshimiwa Naibu Spika, lengo kubwa na maudhui ya Sheria hii ni kuhakikisha kwamba wafanyakazi wote wale ambao wamepata occupation diseases wanatibiwa kupitia mfuko huu; na wale ambao watakuwa wamepata ulemavu uliosababishwa na shughuli za kazi na wenyewe wanaweza kufidiwa au kupata mataibabu kutokana na aina ya ugonjwa walioupata kutokana na ripoti ya madaktari Mheshimiwa Naibu Spika, lakini Serikali sasa inafanyaje? Katika mazingira haya kumtaka mwajiri atimize wajibu wake uko utaratibu ambao uko kwa mujibu wa sheria ambao umewekwa ya kwamba waajiri wote watatakiwa kwanza kuwasilisha michango yao kwa mujibu wa sheria ambapo Sekta Binafsi watatakiwa kuchangia asilimia moja ya wage bill ya kila mwezi, na katika sekta ya umma vilevile asilimia 0.5. sasa kwa wale ambao watakaidi kuchangia maana yake ni kwamba kwanza sheria inasema watatozwa fine ya riba ya asilimia 10 ya kile ambacho wamekichelewesha, lakini pili watapelekwa pia mahakamani na wakithibitika kwamba wameshindwa kuwasilisha michango hiyo adhabu ni kuanzia shilingi milioni 50 au pia kifungo kisichopungua miaka mitano mpaka kumi cha mkuu wa taasisi hiyo.

Name

Abdallah Hamis Ulega

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mkuranga

Primary Question

MHE. DKT. RAPHAEL M. CHEGENI (K.n.y MHE. SALOME W. MAKAMBA) aliuliza:- Wafanyakazi wa migodi ya uchimbaji wa madini hufukuzwa kazi kiholela bila kulipwa fidia stahiki kutokana na ulemavu na magonjwa yanayosababishwa na vitendea kazi hatarishi wakati wakiwa kazini. (a) Je, Serikali iko tayari kuzuia kuingizwa nchini vitendea kazi hatarishi na kufunga migodi ambayo ina wahanga wengi na ulemavu na magonjwa yatokanayo na shughuli za uchimbaji madini? (b) Je, ni lini Serikali itaanza kutumia Sheria ya Fidia Na. 20 ya mwaka 2008 ili wafanyakazi wa migodini walipwe fidia stahiki wanapopata ulemavu au magonjwa wanapokuwa kazini badala ya Sheria ya Fidia ya mwaka 2002? na (c) Je, Serikali inatoa tamko gani kwa waajiri wanaowatelekeza wafanyakazi waliopata ulemavu wakiwa kazini na kukataa kuendelea kulipa gharama za matibabu yao?

Supplementary Question 2

MHE. ABDALLAH H. ULEGA: Mheshimiwa Naibu Spika nashukuru kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali fupi la nyongeza.
Mheshimiwa Naibu Spika, tatizo la wafanyakazi hasa vijana kufukuzwa kazi kiholela, kutokulipwa stahiki pindi wapatapo ajali kazini, kulipwa ujira mdogo sana wa shilingi 4,500 kwa kutwa ya siku, kufanyishwa kazi kwa muda mrefu kinyume cha sheria na taratibu za nchi lipo pia katika Wilaya yangu ya Mkuranga.
Je Serikali ina mpango gani wa kuwalinda vijana hawa wafanyakazi ili waweze kazi zao kuwa ni kazi zenye staha? Ahsante.

Name

Anthony Peter Mavunde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Dodoma mjini

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA WAZIRI MKUU, KAZI, VIJANA NA AJIRA: Mheshimiwa Naibu Spika, kwanza kabisa nataka nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge ya kwamba Serikali kupitia Wizara ya Kazi tumekuwa tukisimamia sana Sheria Namba Sita ya mwaka 2004 ambayo imetoa haki na wajibu kwa wafanyakazi lakini na kwa waajiri pia. Sheria hii imetusaidia sana kutatua migogoro mingi mahali pa kazi, hasa pale inapoonekana sheria hii imekiukwa Serikali imekuwa ikichukua hatua stahiki kama ambavyo imekuwa ikionekana katika mazingira hayo.
Mheshimiwa Naibu Spika, lakini nikija katika swali lake la msingi sasa ya kwamba Serikali tunawalindaje hawa ambao wanafukuzwa kazi kiholela hasa pale wanapoonekana wamepata ulemavu wakiwa kazini.
Mheshimiwa Naibu Spika, kwanza kabisa nimkumbushe tu Mheshimiwa Mbunge kwamba kupata ulemavu ukiwa kazini sio kigezo cha dismissal na kwamba waajiri wote ambao wamekuwa wakikiuka taratibu hiyo ya sheria, sisi kama mamlaka ambayo tunasimamia sheria hizi kazi tumekuwa tukitoa elimu, lakini na kuchukua hatua stahiki.
Mheshimiwa Naibu Spika, lakini pia Mheshimiwa Mbunge nikuhakikishie tu ya kwamba tumekuwa tukiendelea kufanya kaguzi nyingi sana za kazi kwa lengo la kubaini haya mapungufu na tumekuwa tukichukua hatua pindi inapobainika kwamba mwajiri amekiuka sheria hizi. Kwa hiyo, sisi kama Serikali tutaendelea kusimamia Sheria Namba Sita ya mwaka 2004 kuhakikisha kwamba tunalinda haki za wafanyakazi na wafanyakazi hawa basi wasipoteze haki zao zile za kuwa wafanyakazi kwa kufukuzwa tu kiholela na mwajiri; na sisi tutahakikisha kwamba waajiri wote wanafuata sheria za nchi zinavyoelekeza.

Name

Joseph Kasheku Musukuma

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Geita

Primary Question

MHE. DKT. RAPHAEL M. CHEGENI (K.n.y MHE. SALOME W. MAKAMBA) aliuliza:- Wafanyakazi wa migodi ya uchimbaji wa madini hufukuzwa kazi kiholela bila kulipwa fidia stahiki kutokana na ulemavu na magonjwa yanayosababishwa na vitendea kazi hatarishi wakati wakiwa kazini. (a) Je, Serikali iko tayari kuzuia kuingizwa nchini vitendea kazi hatarishi na kufunga migodi ambayo ina wahanga wengi na ulemavu na magonjwa yatokanayo na shughuli za uchimbaji madini? (b) Je, ni lini Serikali itaanza kutumia Sheria ya Fidia Na. 20 ya mwaka 2008 ili wafanyakazi wa migodini walipwe fidia stahiki wanapopata ulemavu au magonjwa wanapokuwa kazini badala ya Sheria ya Fidia ya mwaka 2002? na (c) Je, Serikali inatoa tamko gani kwa waajiri wanaowatelekeza wafanyakazi waliopata ulemavu wakiwa kazini na kukataa kuendelea kulipa gharama za matibabu yao?

Supplementary Question 3

MHE. JOSEPH K. MUSUKUMA: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru. Kwa kuwa swali la msingi limeeleza jinsi watumishi wa migodini wanavyofukuzwa kazi kiholela, pengine wakifanya kazi kwa miaka minane, saba wanafukuzwa kutokana na magonjwa mbalimbali, na Serikali imeondoa fao la kujitoa kwenye Mifuko ya Jamii ikiweka masharti kwamba mpaka miaka 55.
Je, hawa waliofukuzwa kazi wakiwa na miaka tisa na umri wa miaka 40 wanapataje fao lao kwa kusuburi miaka 50 Maana watakuwa na miaka 100?

Name

Anthony Peter Mavunde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Dodoma mjini

Answer

WAZIRI WA NCHI, OFISI YA WAZIRI MKUU, SERA, BUNGE, KAZI, VIJANA, AJIRA NA WATU WENYE ULEMAVU: Mheshimiwa Naibu Spika, Sera ya Hifadhi ya Jamii ambayo inaongoza masuala mazima ya Hifadhi ya Jamii katika nchi yetu ya Tanzania inaendana na Katiba ya nchi kifungu cha 11(1) ambacho Katiba ya nchi yetu inataka jamii kuangalia utaratibu mzima wa kuweka hifadhi ya wananchi na hasa pale wanapofikia umri wa uzeeni ama wanapopata matatizo mengine yoyote. Kwa hiyo, sera hiyo imekuwa ikituongoza kuunda mifuko hii ya Hifadhi ya Jamii kwa ajili ya kutoa kinga wakati wa uzeeni.
Mheshimiwa Naibu Spika, lakini tumepata matatizo ya namna moja ama nyingine. Kadiri uchumi wa Tanzania ulivyoendelea kukua kumeongezeka sekta za kiuchumi ambazo unapata picha kabisa kwamba wafanyakazi ambao wamekuwa wakiajiriwa katika sekta hizo ni lazima watafanya kazi kwa muda mfupi sana, kama katika sekta za migodi, sekta za mashamba na sekta nyinginezo na hivyo basi kumekuwa na namna moja ama nyingine ya kuonekana kabisa kunahitajika kupitia tena sera ya Hifadhi ya Jamii, na kupitia sheria zetu ambazo zinaongoza Mifuko ya Hifadhi ya Jamiii ili kuyapitia mafao yanayotolewa na Mifuko ya Hifadhi ya Jamii. Kusudi la kufanya hivyo ndani ya Serikali ni kutazama kama sera na sheria tulizonazo zitakwenda kujibu matatizo ya wafanyakazi kama wa migodini kutokupata ama kupata fao la kujitoa kwa kuzingatia nature ya kazi zao. Haya yote yataongozwa na mikataba ya Kimataifa na sheria tulizonazo nchini. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, lakini ninaomba nitoe wito kwa Watanzania na wafanyakazi wote watupe subira, na sisi Serikali tuko tunalifanyia kazi suala hili kwa nguvu. Nitoe onyo kwa waajiri wote wanaokiuka matakwa ya kisheria katika kuchangia mifuko ya Hifadhi ya Jamii kwa faida ya wafanyakazi. Na ninaomba niliarifu Bunge lako tukufu, tumeshaunda kikosi kazi chini ya Ofisi ya Waziri Mkuu na tunakaribia kuanza kufanya ukaguzi wa nguvu kwa kuzingatia pia Sheria ya Tanzania Extractive Industries Transparency and Accountability na tutapambana na wale wote wanaofanya udanganyifu katika kuchangia mafao ya wafanyakazi na hasa migodini.

Name

Mariamu Nassoro Kisangi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. DKT. RAPHAEL M. CHEGENI (K.n.y MHE. SALOME W. MAKAMBA) aliuliza:- Wafanyakazi wa migodi ya uchimbaji wa madini hufukuzwa kazi kiholela bila kulipwa fidia stahiki kutokana na ulemavu na magonjwa yanayosababishwa na vitendea kazi hatarishi wakati wakiwa kazini. (a) Je, Serikali iko tayari kuzuia kuingizwa nchini vitendea kazi hatarishi na kufunga migodi ambayo ina wahanga wengi na ulemavu na magonjwa yatokanayo na shughuli za uchimbaji madini? (b) Je, ni lini Serikali itaanza kutumia Sheria ya Fidia Na. 20 ya mwaka 2008 ili wafanyakazi wa migodini walipwe fidia stahiki wanapopata ulemavu au magonjwa wanapokuwa kazini badala ya Sheria ya Fidia ya mwaka 2002? na (c) Je, Serikali inatoa tamko gani kwa waajiri wanaowatelekeza wafanyakazi waliopata ulemavu wakiwa kazini na kukataa kuendelea kulipa gharama za matibabu yao?

Supplementary Question 4

MHE. MARIAM N. KISANGI: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana na mimi kunipa nafasi niweze kuuliza swali moja la nyongeza.
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa kuwa matatizo haya ya wafanyakazi wa migodini yamekuwa yakijirudia mara kwa mara katika Bunge hili, tumekuwa tukiyasikia, nataka kujua.
Je, ni lini sasa Serikali tafanya ukaguzi huo wa makampuni makubwa ya madini na kuwabaini wadanganyifu ambao wanakwepa kuwalipa wafanyakazi mafao yao ya NSSF na kodi nyingine?

Name

Dr. Abdallah Saleh Possi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Nominated

Answer

WAZIRI WA NCHI, OFISI YA WAZIRI MKUU, SERA, BUNGE, KAZI, VIJANA, AJIRA NA WATU WENYE ULEMAVU: Mheshimiwa Naibu Spika, ni kweli kabisa tumegundua kuna udanganyifu mkubwa sana katika migodi na makampuni makubwa ambayo yamekuwa yakihudumu katika nchi yetu ya Tanzania.
Mheshimiwa Naibu Spika, makampuni hayo wakati mwingine yamekuwa yakitoa salary slip mbili, moja ikionesha kiwango cha chini cha malipo ya mshahara na hicho ndicho kinachofanya contribution kwenye Mifuko ya Hifadhi ya Jamii, lakini wana salary slip nyingine ambazo kodi za nchi hazikatwi inavyotakiwa wala mafao ya wafanyakazi hayapelekwi inavyotakiwa.
Naomba nilihakikishie Bunge lako Tukufu, tumegundua tatizo hilo na baada ya muda si mrefu mtasikia kikosi kazi kimeshaundwa kikiwa na wajumbe kutoka Wizara ya Fedha, TRA, Mwanasheria Mkuu, Ofisi ya kwangu - Ofisi ya Kazi, Kamishna Mkuu na watu wengine. Watafanya ukaguzi na kuwabaini hao wote na hatua kali zitachukuliwa na makato hayo yataanza kupelekwa kwa kuzingatia mshahara halisi wa mfanyakazi.