Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Bernadeta Kasabago Mushashu

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. BERNADETA K. MUSHASHU aliuliza: - Je, ni vijiji vingapi havijapatiwa umeme wa REA na nini mpango wa Serikali kusambaza umeme kwenye vijiji vyote vya Mkoa wa Kagera?

Supplementary Question 1

MHE. BERNADETA K. MUSHASHU: Mheshimiwa Mwenyekiti, pamoja na majibu mazuri ya Mheshimiwa Naibu Waziri ninayo maswali mawili ya nyongeza. Hadi sasa maeneo mengi katika Mkoa wa Kagera ambayo yamesambaziwa umeme wa REA umeme umefika tu kwenye ngazi ya vijiji haukuteremka chini. Swali la kwanza, je, ni lini sasa madi wa ujazilizi densification itaweza kuanza Mkoani Kagera ili vijiji vyote sasa na maeneo yote yaliyorukwa na vitongoji yaweze kupatiwa umeme?

Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la pili; katika Mkoa wa Kagera kwenye Manispaa ya Bukoba tunazo Kata kama Kahororo, Buhembe, Nshambya, Nyanga, Kagondo, Kibeta, Kitendaguro na Ijuganyondo ambavyo pamoja na kwamba kata hizo ziko kwenye Manispaa ya Bukoba lakini zimekaa kama vijiji. Je, ni lini sasa Serikali itaanzisha mradi wa Peri- Urban ili sasa vijiji hivi au mitaa hii inayofanana na vijiji iweze kupata umeme wa REA kwa bei nafuu?

Name

Stephen Lujwahuka Byabato

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bukoba Mjini

Answer

NAIBU WAZIRI WA NISHATI: Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kujibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Bernadeta Kasasabago Mushashu, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, ni kweli kwamba kwenye awamu ya kwanza upelekaji wa umeme vijijini tumefika hasa kwenye centres za yale maeneo na ni kwa sababu ya fedha iliyokuwepo.

Mheshimiwa Mwenyekiti, REA III round II peke yake ina shilingi trilioni moja na bilioni mia mbili na hamsini kwa ajili ya kufikisha umeme kwenye vile vijiji vyote ambavyo havikuwa na umeme. Azma na nia ya Serikali ni kuhakikisha kila mtu anapata umeme kwenye eneo lake na tayari nia hiyo imeanza. Tayari uko mradi wa ujazilizi tunaita Densification One ambao unaendelea katika baadhi ya maeneo yetu, lakini tumemaliza tayari upembuzi na kupata wakandarasi, tunaamini kufikia Julai densification 2(b) itaanza, lakini kufikia kwenye Oktoba densification 2(c) itaanza.

Mheshimiwa Mwenyekiti, bado hii haitaweza kumaliza kwa sababu katika hizi densification tuna vitongoji karibu 5,000 na zaidi kidogo. Mnakumbuka hapa tayari Bungeni Mheshimiwa Waziri amesema kwamba tunatafuta mkakati mkubwa wa kuweza kupata fedha nyingi karibia trilioni sita kwa ajili ya kupeleka sasa umeme kwenye vitongoji vyote vilivyobaki nchini ambavyo havina umeme. Kwa hiyo kadri pesa inavyopatikana vitongoji vitazidi kupelekewa umeme kwa kadri Serikali inavyozidi kujipanga.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwenye swali la pili la Peri- Urban, nimshukuru Mheshimiwa Bernadetha kwa kuulizia kuhusu Jimbo la Bukoba Mjini, makofi yalikuwa mengi, swali sikulisikia vizuri, lakini naamini alichokizungumzia ni peri-urban na tayari Serikali imeshatangaza na imefikia hatua za mwisho za kupata wakandarasi wa kupeleka umeme katika maeneo ya mijini lakini yenye uso wa vijiji kama alivyozitaja hizo kata saba za Jimbo la Bukoba Mjini.

Mheshimiwa Mwenyekiti, pia kuna mikoa mingine kama tisa katika awamu hii ya peri-urban nayo kufikia Julai tunaamini mradi huu utaanza kwa ajili ya kufikisha umeme katika maeneo haya kwa ajili ya kupata umeme kwa gharama nafuu.

Name

Ndaisaba George Ruhoro

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ngara

Primary Question

MHE. BERNADETA K. MUSHASHU aliuliza: - Je, ni vijiji vingapi havijapatiwa umeme wa REA na nini mpango wa Serikali kusambaza umeme kwenye vijiji vyote vya Mkoa wa Kagera?

Supplementary Question 2

MHE. NDAISABA G. RUHORO: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru sana kwa fursa hii ya kuuliza swali la nyongeza. Naomba sasa Serikali inijibu, ni kwa nini mkandarasi wa REA Ngara amepotea site, haonekani kwa takribani kipindi cha miezi mitatu? Ahsante. (Makofi)

Name

Stephen Lujwahuka Byabato

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bukoba Mjini

Answer

NAIBU WAZIRI WA NISHATI: Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Ndaisaba, Mbunge wa Ngara, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, awamu ya upelekaji wa umeme vijijini iko na awamu tofautitofauti, kama nilivyosema kwenye jibu la msingi kuna upembuzi yakinifu, ku-survey yake maeneo, uagizaji wa vifaa na hatua ya mwisho ya uwekaji wa miundombinu yenyewe. Maeneo hayo na mazingira hayo ya hatua hizo yanaweza kufanya mkandarasi asionekane site kwa muda na hasa pale anapokuwa kwenye hatua ya kuagiza vifaa. Naamini maeneo mengi wengine vifaa vimefika, wengine bado, kwa hiyo sehemu ambapo hajafika, naamini itakuwa labda alichelewa kwenye kuagiza vifaa, lakini vifaa vitafika, kwa sababu maelekezo yetu ni kabla ya Desemba mwaka huu miradi iwe imekamilika.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nichukue nafasi hii kuwaelekeza wakandarasi wote kuendelea na kazi katika site zao kulingana na schedule walizoziweka na vifaa vilivyopo ili tuweze kufikia deadline ya Desemba kuweza kufikisha umeme kwenye maeneo hayo.

Name

Rashid Abdallah Shangazi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mlalo

Primary Question

MHE. BERNADETA K. MUSHASHU aliuliza: - Je, ni vijiji vingapi havijapatiwa umeme wa REA na nini mpango wa Serikali kusambaza umeme kwenye vijiji vyote vya Mkoa wa Kagera?

Supplementary Question 3

MHE. RASHID A. SHANGAZI: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante. Kata ya Mbaramo na Shagayo katika Jimbo la Mlalo bado hakuna hata kijiji kimoja kimesambaziwa umeme. Nataka kujua, ni lini Serikali itaanza usambazaji wa umeme katika kata hizo?

Name

Stephen Lujwahuka Byabato

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bukoba Mjini

Answer

NAIBU WAZIRI WA NISHATI: Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Shangazi, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, Mkoa wa Tanga unao wakandarasi watatu wanaopeleka umeme vijijini na katika Jimbo lake yuko Mkandarasi anaitwa Dem Electric ambaye anapeleka umeme katika maeneo hayo. Nafahamu kwamba mkandarasi huyu anajitahidi kufanya kazi zake vizuri na atakuwepo kwenye maeneo ya kazi, pengine ameanzia eneo lingine ili aje amalizie kwenye hayo maeneo ya kata alizozisema za Mbaramo na Shagayo kama nitakuwa nimezitaja vizuri. Nichukue nafasi hii kumwelekeza yeye pamoja na wakandarasi wengine wagawanye magenge wanayotumia katika kufanya kazi ili kila eneo la Mbunge liweze kuonekana likiwa linafanyiwa kazi kama ambavyo walienda wakaripoti wakaanza kufanya kazi za utekelezaji katika maeneo hayo na eneo hilo liwe mojawapo la kuhakikisha kwamba wanatoka kwenye maeneo waliyofikia sasa kwenda kwenye maeneo mengine ili kufanya kazi na kukamilisha kazi kwa wakati.

Name

Saashisha Elinikyo Mafuwe

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Hai

Primary Question

MHE. BERNADETA K. MUSHASHU aliuliza: - Je, ni vijiji vingapi havijapatiwa umeme wa REA na nini mpango wa Serikali kusambaza umeme kwenye vijiji vyote vya Mkoa wa Kagera?

Supplementary Question 4

MHE. SAASHISHA E. MAFUWE: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana kwa kuniona. Kwa kuwa Jimbo la Hai kuna changamoto kubwa sana ya uchakavu wa miundombinu, lakini kumekuwa na maombi ya muda mrefu sana ya wananchi tangia mwaka 2008 mpaka sasa hivi hawajaunganishiwa; na kwa kuwa tulikaa na Mheshimiwa Waziri na timu yake na wakapeleka wataalam kule Hai kwenda kubaini mahitaji ya wananchi. Je, ni lini Serikali itatuletea vifaa ili wananchi waweze kuunganishiwa umeme na kurekebisha miundombinu?

Name

Stephen Lujwahuka Byabato

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bukoba Mjini

Answer

NAIBU WAZIRI WA NISHATI: Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Saashisha, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, ni kweli Mheshimiwa Saashisha amefuatilia sana umeme katika jimbo lake na kama alivyosema Mheshimiwa Waziri alituma timu kwenda kufuatilia. Niombe kwamba baada ya hapa tukutane ili nipate taarifa ya hiyo Kamati na nitoe maelekezo ya kufanya kile ambacho kilibainika kinaweza kufanyika ili tatizo lake la muda mrefu ambalo amekuwa ukilifuatilia liweze kutatuliwa. Naomba baada ya hapa tuweze kuwasiliana.