Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 7 Sitting 18 Energy and Minerals Wizara ya Nishat 157 2022-05-09

Name

Bernadeta Kasabago Mushashu

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. BERNADETA K. MUSHASHU aliuliza: -

Je, ni vijiji vingapi havijapatiwa umeme wa REA na nini mpango wa Serikali kusambaza umeme kwenye vijiji vyote vya Mkoa wa Kagera?

Name

Stephen Lujwahuka Byabato

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bukoba Mjini

Answer

NAIBU WAZIRI WA NISHATI alijibu: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Waziri wa Nishati, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Bernadeta Kasabago Mushashu, Mbunge wa Viti Maalum, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, Mkoa wa Kagera una vijiji 662, ambapo kati ya hivyo, vijiji 139 havijafikiwa na miundombinu ya umeme. Vijiji vyote 139 vilivyobaki vitapatiwa umeme kupitia utekelezaji wa Mradi wa Umeme Vijijini Awamu ya Tatu – Mzunguko wa Pili unaoendelea. Mkandarasi ambaye ni Joint Venture wa kampuni za M/S JV Pomy Engineering Company Limited na Qwihaya General Enterprises Company Limited ndiyo wanaotekeleza mradi huo kwa Mkoa wa Kagera. Gharama ya mradi ni Shilingi Bilioni 34.078.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kazi za mradi zinahusisha ujenzi wa kilomita 812 za njia za umeme msongo wa kilovoti 33, ufungaji wa mashine umba 176, ujenzi wa kilomita 139 ya miundombinu ya usambazaji ya msongo wa voti 400 na uunganishaji wa wateja wa awali wapatao 3,058. Utekelezaji wa mradi umeshaanza kwa mkandarasi kukamilisha upimaji na usanifu wa kina na kuanza uagizaji wa vifaa vya utekelezaji. Mradi unatarajiwa kukamilika ifikapo Desemba, 2022.