Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Ritta Enespher Kabati

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. DKT. RITTA E. KABATI K.n.y. MHE. JESCA J. MSAMBATAVANGU aliuliza: - Je, Serikali ina mpango gani mahsusi wa kurudisha uoto wa asili wa milima ya Iringa ili kuendelea kutunza mazingira yake na vyanzo vya maji?

Supplementary Question 1

MHE. DKT. RITTA E. KABATI: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante kwa kunipa nafasi niulize maswali madogo ya nyongeza. Ninamshukuru Mheshimiwa Waziri kwa majibu yake mazuri

Mheshimiwa Mwenyekiti, kumekuwa kuna vikundi ambavyo vimekuwa vikijishughulisha na utunzaji wa mazingira na yeye mwenyewe amekiri hata wanafunzi wameendelea kufungua program zao. Changamoto kubwa vikundi hivi vinakuwa vina ukosefu wa fedha ili viweze kufanya vizuri zaidi.

Je, Serikali inawasaidiaje, vikundi hivi viendelee kupanda miti mingi na kuendelea kutunza mazingira ambayo wanayaishi?

Swali la pili, ili kupunguza shughuli za kibinadamu kuzunguka milima na vyanzo vya maji.

Je, Serikali ina mpango gani wa kuwezesha kufanya shughuli zingine kama za ufugaji, uvuvi, katika maeneo ambayo wanazunguka wananchi?

Name

Khamis Hamza Khamis

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Uzini

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA MAKAMU WA RAIS - MUUNGANO NA MAZINGIRA: Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kujibu maswali mawili ya Mheshimiwa Dkt. Ritta Kabati kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali inatambua uwepo wa vikundi mbalimbali ambavyo vinahitaji kusaidiwa, lakini tunajiridhisha na kuangalia umuhimu wa vikundi hivyo na kwa kiasi gani wanasaidia na wao katika kuimarisha mazingira ndani ya milima lakini na vyanzo vya maji. Serikali ipo tayari kabisa kuwasaidia vikundi hivyo kwa ajili ya kuimarisha mazingira yetu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, swali lake la pili, namna gani tutawezesha, tutawezesha kwa kuwapatia taaluma mbalimbali na kuwaita katika mikutano yetu ili kuwapa taaluma kwa ajili ya kuimarisha mazingira ndani ya nchi yetu.

Name

Shally Josepha Raymond

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. DKT. RITTA E. KABATI K.n.y. MHE. JESCA J. MSAMBATAVANGU aliuliza: - Je, Serikali ina mpango gani mahsusi wa kurudisha uoto wa asili wa milima ya Iringa ili kuendelea kutunza mazingira yake na vyanzo vya maji?

Supplementary Question 2

MHE. SHALLY J. RAYMOND: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana. Tatizo lililo kwenye milima ya Iringa linafanana kabisa na tatizo lililoko tambarare ya Mlima wa Kilimanjaro kwa ajili ya mabadiliko ya tabia nchi. Je, Serikali itaungana lini na wanawake wa Mkoa wa Kilimanjaro, ambao wako tayari sana kurejesha uoto huo kwa kuotesha miti katika vihamba vyao, hususani miti ya matunda? (Makofi)

Name

Khamis Hamza Khamis

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Uzini

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA MAKAMU WA RAIS - MUUNGANO NA MAZINGIRA: Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kujibu swali la Mbunge kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, suala lake ni kweli tunajua kwamba wanawake ama vikundi mbalimbali wakiwemo wanawake, wanaimarisha sana suala la mazingira kwa upandaji miti, pamoja na na miti ya matunda. Serikali inaahidi kutoa motisha kwa wale ambao watafanya vizuri kwenye kampeni yetu kapambe ambayo itamalizika tarehe 30 Juni.

Name

Asha Abdullah Juma

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. DKT. RITTA E. KABATI K.n.y. MHE. JESCA J. MSAMBATAVANGU aliuliza: - Je, Serikali ina mpango gani mahsusi wa kurudisha uoto wa asili wa milima ya Iringa ili kuendelea kutunza mazingira yake na vyanzo vya maji?

Supplementary Question 3

MHE. ASHA ABDULLAH JUMA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante. Kwa kuwa uharibifu huu unaofanyika kwenye milima, uko vilevile kwenye fukwe za bahari na zile sehemu ambazo bahari inaungana na mito. Mikoko inazidi kukatwa, kila kukicha na hivyo kuharibu mazingira na sehemu za kuzalia viumbe vya majini.

Je, Serikali sasa itakuja na program gani ya kuongeza hamasa katika kupanda mikoko katika sehemu hizo ili kunusuru mazingira hayo.(Makofi)

Name

Khamis Hamza Khamis

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Uzini

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA MAKAMU WA RAIS - MUUNGANO NA MAZINGIRA: Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Asha maarufu kwa jina la ‘Mshua’ kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali ina mpango mkakati ambao wananchi wote ambao wanasaidia kupanda mikoko kando kando ya bahari, wanakuwa na taaluma maalum lakini wanapewa motisha. Kwa mfano, Bagamoyo, Zanzibar, ziko sehemu ambazo tayari wameshapanda mikoko na wale ambao wamepanda mikoko well na ikawa inahuika, basi Serikali tunawapa motisha na kufuatilia siku hadi siku. (Makofi)

Name

Sophia Hebron Mwakagenda

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. DKT. RITTA E. KABATI K.n.y. MHE. JESCA J. MSAMBATAVANGU aliuliza: - Je, Serikali ina mpango gani mahsusi wa kurudisha uoto wa asili wa milima ya Iringa ili kuendelea kutunza mazingira yake na vyanzo vya maji?

Supplementary Question 4

MHE. SOPHIA H. MWAKAGENDA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana, kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali la nyongeza.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Mheshimiwa Waziri katika Wilaya ya Rungwe kuna sehemu ya chanzo cha maji cha Kijungu ambayo inapeleka kwenye daraja la Mungu maji yanayoenda kwenye Mto wa Kiwira. Serikali imeacha kwa muda mrefu sana kuweka mazingira na kuhakikisha chanzo hiki kinakuwa salama na kuendelea kuwa historia ya Wilaya ya Rungwe.

Je, ni lini mtapeleka fedha na kuhakikisha mnalinda eneo lile linakuwa salama na linaendelea kuwa kivutio kwa Watanzania na wageni wanaokuja pale?

Name

Khamis Hamza Khamis

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Uzini

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA MAKAMU WA RAIS - MUUNGANO NA MAZINGIRA: Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kujibu la Mheshimiwa Sophia kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, katika bajeti ambayo imewekwa ya ofisi yetu basi sehemu hii ambayo umeitaja Mheshimiwa tumeichukua na ndani ya bajeti yetu ipo na tutatekeleza mara baada tu ya kikao hiki cha bajeti. (Makofi)