Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 7 Sitting 18 Enviroment Ofisi ya Makamu wa Rais Mazingira na Muungano 153 2022-05-09

Name

Jesca Jonathani Msambatavangu

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Iringa Mjini

Primary Question

MHE. DKT. RITTA E. KABATI K.n.y. MHE. JESCA J. MSAMBATAVANGU aliuliza: -

Je, Serikali ina mpango gani mahsusi wa kurudisha uoto wa asili wa milima ya Iringa ili kuendelea kutunza mazingira yake na vyanzo vya maji?

Name

Khamis Hamza Khamis

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Uzini

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA MAKAMU WA RAIS, MUUNGANO NA MAZINGIRA alijibu: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Makamu wa Rais, Muungano na Maiznigra, naomba Kujibu swali la Mheshimiwa Jesca Jonathan Msambatavangu, Mbunge wa Iringa Mjini kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali imebaini kuwepo kwa uharibifu wa mazingira unaotokana na uvamizi wa wananchi wanaofanya shughuli za kibinadamu kwenye milima na vyanzo vya maji katika Wilaya ya Iringa Mjini pamoja na Wilaya nyingine Mkoa wa Iringa. Kutokana na changamoto hiyo, Mkoa wa Iringa umeanzisha programu ya upandaji miti kwenye maeneo yaliyoharibiwa ambapo kila Kata imepanda miti 1,000 kwa mwaka ili kuokoa maeneo yaliyoharibiwa.

Mheshimiwa Mwenyekiti, aidha, programu hii imeimarishwa zaidi na uzinduzi wa kampeni ya ‘Soma na Mti’ iliyozinduliwa na Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais (Muungano na Mazingira) Mheshimiwa Dkt. Selemani Saidi Jafo tarehe 25 Januari, 2022 katika Shule ya Sekondari ya Wasichana ya Iringa. Kampeni hii imehamasisha shule za Msingi na Sekondari za Mkoa wa Iringa kupanda miti takribani 27,656 katika maeneo mbalimbali ikiwemo shule vyanzo vya maji, mabonde, miteremko ya milima na kandokando ya barabara.

Mheshimiwa Mwenyekiti, ili kuhakikisha mazingira ya milima na vyanzo vya maji katika Mkoa wa Iringa yanastawi Ofisi ya Mkoa wa Iringa inaendelea kuotesha vitalu vya miche Laki Tatu kila mwaka na kuwapatia wananchi wa mkoa wa Iringa kuipanda katika maeneo yao. (Makofi)