Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Eng. Ezra John Chiwelesa

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Biharamulo Magharibi

Primary Question

MHE. ENG. EZRA J. CHIWELESA aliuliza: - Je, ni lini Serikali itarejesha fedha Shilingi milioni 204 iliyorudishwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 ili iweze kukamilisha ujenzi wa Hospitali ya Wilaya ya Biharamulo?

Supplementary Question 1

MHE. ENG. EZRA J. CHIWELESA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru, labda sasa niseme jambo moja, leo ni mara yangu ya tatu nauliza swali hili hili. Mwaka jana kwenye Bunge la bajeti nilijibiwa hivi hivi. Mwaka huu pia Wizara ya Fedha imenijibu kwamba inashughulikia. Ila nimekuwa disappointed na majibu ya Serikali kwa sababu wanasema Wilaya ya Biharamuo haikufuata utaratibu.

Mheshimiwa Mwennyekiti, nina barua hapa ya tarehe 9 Juni, 2020, copy ninayo na ninaamini kila sehemu ipo. Nina barua hapa ya tarehe 20 Agosti, 2020 copy ninayo na barua ipo. Sasa kinachoshangaza ni kwamba, majibu niliyopewa na Wizara hii hii mwaka jana ni tofauti na majibu ninayopewa leo. Nilikuwa naona kwamba tumeshaenda mbele, lakini majibu nayojibiwa leo wananirudisha nyuma tena. Sasa nina maswali mawili ya nyongeza, naomba Serikali inipe majibu hapa wananchi wa Biharamulo wakiwa wamesubiria hospitali kwa muda mrefu.

Ni lini fedha hii inapelekwa? Yaani lini siyo nyuma wala mbele lini, date, kabla ya mwisho wa bajeti hii?

Mheshimiwa Mwenyekiti, lakini pili tuna pesa milioni 376 kwa ajili ya vifaa tiba ya hospitali hii. Sasa, leo ni mwezi wa tano, mwaka wa fedha unaisha. Kwa hiyo tusiletewe hii fedha mwezi wa sita katikati tukaambiwa inatakiwa itumike kwa haraka. Pamoja na hii nijue fedha ya vifaa tiba inakuja lini, na utaratibu wake ukoje kama kama inachelewa tunairudisha au tunabaki nayo? Majibu mawili tu.

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE): Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kujibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Engineer Ezra John Chiwelesa, Mbunge wa Jimbo la Biharamulo Magharibi kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba Serikali inafanya kazi kwa kufuata kumbukumbu ambazo zinaoneshwa katika mafaili yetu lakini katika document mbalimbali za Serikali. Na sisi tumefuatilia Wizara ya Fedha na Mipango; pamoja na kwamba Mheshimiwa Mbunge una hizo barua inawezekana ziliandikwa lakini hatuzioni Wizara ya Fedha na Mipango, na suala lilikuwa sio kuandika barua ilikuwa barua zifikishwe Wizara ya Fedha na Mipango.

Kwa hiyo, kama waliandika kwa ku-back date, ili kuweza kutengeneza mazingira hayo sisi hatujazipata hizo, na tungezipata nikuhakikishie Serikali Sikivu ingezifanyia kazi. Kwa hiyo, nikuhakikishie Mheshimiwa Mbunge, tunachosema hapa ni sahihi na tunaendelea kusema vitu sahihi katika Bunge hili Tukufu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kuhusiana na lini fedha hizi zinapelekwa katika mwaka huu wa fedha tayari mmepata milioni 300 kwa ajili ya ujenzi wa hospitali ya Halmashauri ya Biharamulo. Mwaka ujao wa fedha mmepata milioni 750 kwa ajili ya ujenzi wa hospitali hiyo. Kwa hiyo, hapa ni wazi kwamba Serikali inaendelea kupeleka fedha na hospitali inaendelea kujengwa. Hitaji la wananchi ni hospitali na Serikali ina commitment kubwa kuhakikisha hospitali inaendelea kujengwa.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kuhusiana na milioni 376 za vifaa tiba utaratibu upo wazi tunatepeleka fedha Bohari Kuu ya Madawa (MSD) na itanunua vifaa vile ambavyo imeorodheshwa na halmashauri vitaletwa kwa ajili ya huduma hizo. Nikuhakikishie tu, kwamba MSD inakwenda vizuri sana, vifaa vitakuja huduma zitaendelea pale Biharamulo.

Name

Yahaya Omary Massare

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Manyoni Magharibi

Primary Question

MHE. ENG. EZRA J. CHIWELESA aliuliza: - Je, ni lini Serikali itarejesha fedha Shilingi milioni 204 iliyorudishwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 ili iweze kukamilisha ujenzi wa Hospitali ya Wilaya ya Biharamulo?

Supplementary Question 2

MHE. YAHAYA O. MASSARE: Mheshimiwa Mwenyekiti; iko dhamira ya Serikali ya kujenga hospitali za halmashauri 28 katika bajeti ambayo tunaimaliza sasa. Je, lini hospitali hizi zitapelekewa fedha, ikiwemo hospitali ya Halmashauri ya Itigi?

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE): Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Massare, Mbunge wa Manyoni kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, hospitali zote za halmashauri zote ambazo zimeanza ujenzi na vituo vyote vya afya ambavyo vimeanza ujenzi kwa fedha ya Serikali mpango wa Serikali ni kuendelea kupeleka fedha kwa ajili ya ukamilishaji wa hopitali hizo. Ndiyo maana kwenye mwaka ujao wa fedha tumetenga zaidi ya shilingi bilioni 69.95 kwa ajili ya ukamilishaji wa hospitali zile 59, ikiwemo hii ambayo Mheshimiwa Massare ameisema. Ahsante.