Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 7 Sitting 18 Regional Administration and Local Government Authorities Ofisi ya Rais TAMISEMI. 152 2022-05-09

Name

Eng. Ezra John Chiwelesa

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Biharamulo Magharibi

Primary Question

MHE. ENG. EZRA J. CHIWELESA aliuliza: -

Je, ni lini Serikali itarejesha fedha Shilingi milioni 204 iliyorudishwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 ili iweze kukamilisha ujenzi wa Hospitali ya Wilaya ya Biharamulo?

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE) alijibu: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais-TAMISEMI naomba kujibu swali la Mheshimiwa Eng. Ezra John Chiwelesa Mbunge wa Jimbo la Biharamulo Magharibi kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali kupitia Sheria ya Bajeti Na. 11 ya Mwaka 2015 na kanuni zake iliweka utaratibu kwa halmashauri zote nchi, kuomba kibali Wizara ya Fedha na Mipango kwa fedha za miradi zinazotarajiwa kuvuka mwaka wa fedha husika kurejeshwa mfuko mkuu wa Serikali. Maombi hayo yalipaswa kufanyika siku 15 kabla ya tarehe 30 Juni ya mwaka husika.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Halmashauri ya Wilaya ya Biharamulo haikufuata utaratibu huo. Hivyo, hali hiyo ilisababisha fedha hizo kurejeshwa katika mfuko mkuu wa Serikali. Aidha, katika mwaka wa fedha 2021/2022 Serikali ilipeleka shilingi milioni 300 kwa ajili ya kuendelea na ujenzi wa hospitali hiyo, na katika mwaka wa fedha 2022/2023, Serikali imetenga shilingi milioni 750 kwa ajili ya ujenzi wa hospitali hiyo. Ahsante.