Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Jonas William Mbunda

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mbinga Mjini

Primary Question

MHE. JONAS W. MBUNDA aliuliza: - Je, ni lini Serikali itaanza ujenzi wa Vituo vya Dawati la Jinsia katika kila Makao Makuu ya Polisi ya Wilaya?

Supplementary Question 1

MHE. JONAS W. MBUNDA: Mheshimiwa Spika, namshukuru Naibu Waziri kwa majibu mazuri ya Serikali. Vitendo vya ukatili na unyanyasaji wa kijinsia unaendelea katika nchi yetu, kuna umuhimu mkubwa wa Serikali kuweka mikakati ya kuhakikisha kwamba vituo hivyo vinajengwa kwa nchi nzima.

Mheshimiwa Spika, jengo la dawati la jinsia lililoanza kujengwa katika Wilaya ya Mbinga sehemu kubwa limejengwa kupitia michango ya wadau mbalimbali. Swali langu: Je, Serikali ni lini italeta fedha kuhakikisha kwamba inakamilisha ujenzi wa jengo hilo? (Makofi)

Name

Sagini Jumanne Abdallah

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Butiama

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI: Mheshimiwa Spika, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Mbunda, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, kama nilivyosema katika jibu la msingi, vyanzo vya fedha kwa ajili ya ujenzi wa vituo vya Polisi vikiwemo maeneo ya jinsia na watoto zinatoka Serikalini, kwa wadau wa ndani na wa nje na mashirika mbalimbali. Kwa hiyo, nampongeza Mheshimiwa Mbunda kwa wadau wake kushiriki, lakini tumesema pale ambapo watakuwa wamefika kiwango cha umaliziaji kupitia Mfuko wa Tuzo na Tozo ya Jeshi la Polisi, tutasaidia kukamilisha.

Mheshimiwa Spika, kwa hiyo, niko tayari kuwasiliana nawe ili kuona nini kinahitajika kukamilisha kituo hicho alichokirejea.

Mheshimiwa Spika, ahsante.