Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 7 Sitting 16 Home Affairs Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi 137 2022-05-05

Name

Jonas William Mbunda

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mbinga Mjini

Primary Question

MHE. JONAS W. MBUNDA aliuliza: -

Je, ni lini Serikali itaanza ujenzi wa Vituo vya Dawati la Jinsia katika kila Makao Makuu ya Polisi ya Wilaya?

Name

Sagini Jumanne Abdallah

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Butiama

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI alijibu: -

Kwa niaba ya Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Jonas William Mbunda, Mbunge wa Mbinga Mjini, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, Serikali inatambua umuhimu wa Dawati la Jinsia na Watoto kuwepo kwenye vituo vya Polisi nchini, kwani husaidia kushughulikia matatizo ya wananchi wa makundi yanayonyanyaswa katika jamii wakiwemo wanawake na watoto. Ujenzi wa ofisi za dawati katika vituo vya Polisi unaendelea nchi nzima na kwa kadri ya upatikanaji wa fedha Serikalini, Mashirika ya Kimataifa na Wadau wa Maendeleo wa ndani na nje ya nchi.

Mheshimiwa Spika, mpaka sasa zimejengwa ofisi 70 katika vituo vya Polisi na vinafanya kazi. Kwa Mkoa wa Ruvuma, vituo vya dawati la jinsia na watoto vimejengwa kwenye vituo vya Polisi Songea, Tunduru na Mbinga. Aidha, ramani za majengo ya vituo vya Polisi zimeboreshwa ili kuingiza ofisi za jinsia na watoto. Hivyo, vituo vipya vitakavyokuwa vinavyojengwa kuanzia sasa vitakuwa

vimezingatia umuhimu wa kuwa na Ofisi za Dawati la Jinsia na Watoto.

Mheshimiwa Spika, nashukuru.