Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Shabani Omari Shekilindi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Lushoto

Primary Question

MHE. SHABANI O. SHEKILINDI aliuliza: - Je, ni lini maeneo mengi ya Mji wa Lushoto yatapimwa?

Supplementary Question 1

MHE. SHABANI O. SHEKILINDI: Mheshimiwa Spika, namshukuru Waziri kwa majibu mazuri, lakini pia nimshukuru kwa kutupa milioni 2008. Kama unavyojua Wilaya ya Lushoto ni kubwa sana. Kwa hiyo, milioni 208 ni fedha chache sana. Swali la kwanza, je, Serikali haiona sasa kwamba kuna haja ya kuongeza fedha zile angalau zifike hata bilioni moja ili kumaliza upimaji katika Wilaya ya Lushoto?

Mheshimiwa Spika, swali la pili; takwimu za nchi nzima zinaonesha kwamba ni asilimia 25 tu ya sehemu ya ardhi ndiyo iliyopimwa katika nchi hii ya Tanzania. Je, haioni Serikali kwamba inasuasua sana kwa suala hili la kupima na kuleta migogoro ndani ya nchi hii. Sasa Serikali ina mpango gani au ina mkakati gani wa haraka kuhakikisha kwamba inatenga bajeti ya kutosha na kupima ardhi hii nchi nzima ili kuondoa migogoro ndani ya nchi hii ya Tanzania? (Makofi)

Name

Ridhiwani Jakaya Kikwete

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chalinze

Answer

NAIBU WAZIRI WA ARDHI, NYUMBA NA MAENDELEO YA MAKAZI: Mheshimiwa Spika, naomba kumjibu maswali ya nyongeza Mheshimiwa Shekilindi, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, kwanza Serikali imeendelea ku-support hatua mbalimbali zanazofanywa na halmashauri zetu kuhakikisha kwamba miradi au maeneo yetu yanapimwa. Katika kufanya hivyo Serikali imepata mkopo wa dola milioni 150 kwa ajili ya utekelezaji wa mradi wa umilikishaji wa ardhi ambapo katika moja ya mambo makubwa yanayoenda kufanyika ni kuendelea kupima na kupanga ardhi ya Tanzania. Nataka nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba pamoja na kwamba anaona fedha hizi hazitoshi lakini mipango kwa ajili ya kupima Tanzania nayo pia inaendelea.

Mheshimiwa Spika, pili, katika ardhi ya Tanzania, takribani asilimia 20 ya maeneo ya Tanzania yamepimwa ambapo viwanja zaidi ya 2,800 na mashamba zaidi ya 28,000 yamekwisha tambulika. Hivyo nataka nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba zoezi linaendelea kufanyika na ni mipango na maelekezo ya Serikali kuhakikisha kwamba ardhi yote ya Tanzania inapimwa. Ahsante.