Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 7 Sitting 16 Lands, Housing and Human Settlement Development Wizara ya Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi 135 2022-05-05

Name

Shabani Omari Shekilindi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Lushoto

Primary Question

MHE. SHABANI O. SHEKILINDI aliuliza: -

Je, ni lini maeneo mengi ya Mji wa Lushoto yatapimwa?

Name

Ridhiwani Jakaya Kikwete

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chalinze

Answer

NAIBU WAZIRI WA ARDHI, NYUMBA NA MAENDELEO YA MAKAZI alijibu: -

Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Shabani Omari Shekilindi, Mbunge wa Lushoto, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, halmashauri ni mamlaka ya upangaji kwa mujibu wa Sheria ya Mipango Miji Na. 8 ya mwaka 2007, hivyo majukumu ya kisheria ya kutenga bajeti, kwa ajili ya kupanga na kupima yapo ndani yao. Hata hivyo, katika mwaka wa fedha 2021/2022, Serikali imetoa mkopo wenye thamani ya shilingi bilioni 55.6 kwa halmashauri 55, Vyuo vya Ardhi vya Tabora na Morogoro na Chuo Kikuu Ardhi Dar es Salaam, kwa ajili ya utekelezaji wa Programu ya Kupanga, Kupima na Kumilikisha Ardhi.

Mheshimiwa Spika, Halmashauri ya Wilaya ya Lushoto ni miongoni mwa halmashauri zilizokopeshwa fedha hizo ambapo jumla ya shilingi milioni 208 zimetolewa kwa ajili ya kupima viwanja takriban 2,600 katika maeneo ya Lushoto Mjini, Mnazi, Mlola, Mlalo na Lukozi. Pamoja na jitihada hizi za Serikali, natoa rai kwa Halmashauri ya Wilaya ya Lushoto na Halmashuri zote nchini kuhakikisha kuwa zinatenga fedha katika bajeti zao kwa ajili ya kupanga, kupima na kumilikisha ardhi.