Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Emmanuel Adamson Mwakasaka

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tabora Mjini

Primary Question

MHE. EMMANUEL A. MWAKASAKA K.n.y. MHE. SEIF K. S. GULAMALI aliuliza: - Je, Serikali ina mpango gani wa kugawa Mkoa wa Tabora na kupata Mkoa wa Manonga ili kurahisisha shughuli za kiutawala na kiuchumi?

Supplementary Question 1

MHE. EMMANUEL A. MWAKASAKA: Mheshimiwa Spika, ahsante.

Mheshimiwa Spika, kwa kuwa suala hili la kugawa Mkoa wa Tabora na kuwa na Mkoa unaitwa Manonga ni la muda mrefu sasa na michakato mingi ilishafanywa ikiwemo jina lenyewe la Manonga. Pamoja na majibu mazuri ya Serikali, Je, hicho kikao cha tarehe 22 kama alivyosema Mheshimiwa Waziri cha RCC kikifanyika, Serikali iko tayari kuugawa Mkoa huu wa Tabora?

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE): Mheshimiwa Spika, ahsante sana. Naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Emmanuel Mwakasaka Mbunge wa Tabora Mjini, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, Serikali imetoa maelekezo na sheria kwamba lazima taratibu hizo zifuatwe na kisha maombi hayo yawasilishwe rasmi Ofisi ya Rais, TAMISEMI ili iweze kuwasilishwa kwenye mamlaka husika baada ya tathmini. Kwa hiyo, nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge baada ya wao kuwasilisha Ofisi ya Rais, TAMISEMI, ofisi itafanya tathmini na kuwasilisha mamlaka husika ili maamuzi yaweze kufanyika kwa kadri itakavyoona inafaa, ahsante.

Name

Benaya Liuka Kapinga

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mbinga Vijijini

Primary Question

MHE. EMMANUEL A. MWAKASAKA K.n.y. MHE. SEIF K. S. GULAMALI aliuliza: - Je, Serikali ina mpango gani wa kugawa Mkoa wa Tabora na kupata Mkoa wa Manonga ili kurahisisha shughuli za kiutawala na kiuchumi?

Supplementary Question 2

MHE. BENAYA L. KAPINGA: Mheshimiwa Spika, nakushukuru sana.

Mheshimiwa Spika, Halmashauri ya Mbinga Vijijini, Jimbo la Mbinga Vijijini kutokana na ukubwa wake tulipata ahadi ya Serikali ya kuligawa. Je, ni lini ahadi hiyo itatekelezwa?

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE): Mheshimiwa Spika, ahsante sana. Naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Benaya Kapinga Mbunge wa Jimbo la Mbinga Vijijini, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, ninawaomba Jimbo la Mbinga kwa maana ya Halmashauri ya Mbinga wapitie hatua zile kwa mujibu wa sheria, wawasilishe hayo maombi Ofisi ya Rais, TAMISEMI, tutafanya tathmini lakini tutawapa mrejesho baada ya kufanya tathmini na hatimaye tutawasilisha kwa mamlaka husika, ahsante. (Makofi)