Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 7 Sitting 16 Regional Administration and Local Government Authorities Ofisi ya Rais TAMISEMI. 131 2022-05-05

Name

Seif Khamis Said Gulamali

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Manonga

Primary Question

MHE. EMMANUEL A. MWAKASAKA K.n.y. MHE. SEIF K. S. GULAMALI aliuliza: -

Je, Serikali ina mpango gani wa kugawa Mkoa wa Tabora na kupata Mkoa wa Manonga ili kurahisisha shughuli za kiutawala na kiuchumi?

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE) alijibu: -

Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, TAMISEMI, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Seif Khamis Said Gulamali, Mbunge wa Jimbo la Manonga kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, utaratibu wa kuanzisha Mkoa, Wilaya na Tarafa mpya umebainishwa kupitia Sheria ya Uanzishwaji wa Mikoa na Wilaya na Mwongozo wa Uanzishwaji wa Maeneo ya Utawala wa mwaka 2014.

Mheshimwa Spika, kwa mujibu wa Sheria hii maombi ya kuanzishwa Mkoa mpya hupata ridhaa ya vijiji, kamati za maendeleo za kata, mabaraza ya Madiwani ya halmashauri zilizomo katika mkoa, Kamati ya Ushauri ya Wilaya (DCC) na Kamati ya Ushauri ya Mkoa (RCC) ya Mkoa Mama.

Mheshimiwa Spika, katika Kikao cha Kamati ya Ushauri ya Mkoa (RCC) cha tarehe 3 Machi, 2022 yaliwasilishwa mapendekezo ya kugawa Mkoa wa Tabora, ambapo ilipendekezwa suala hilo kuwasilishwa katika kikao Maalum cha Kamati ya Ushauri ya Mkoa (RCC) kitakachofanyika Mei, 2022.

Mheshimiwa Spika, Ofisi ya Rais TAMISEMI itakapopokea mapendekezo hayo, itafanya uhakiki na tathmini kisha itawayasilisha katika Mamlaka husika kwa ajili ya maamuzi kadiri itakavyoona inafaa.