Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Deo Kasenyenda Sanga

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Makambako

Primary Question

MHE. DEO K. SANGA aliuliza: - Je ni lini Serikali itaangalia upya mipaka ya kiutawala katika Jimbo la Makambako?

Supplementary Question 1

MHE. DEO K. SANGA: Mheshimiwa Spika, nakushukuru kwa majibu mazuri ya Serikali; hata hivyo, nina swali moja la nyongeza.

Mheshimiwa Spika, kwa kuwa majibu ni mazuri na kwa kuwa wananchi wa Makambako eneo la kiutawala kama alivyojibu kwenye swali la msingi. Ni lini sasa Serikali pamoja na Tume hiyo Tukishiikiana mimi na Serikali tutakwenda kwenye Tume ili jambo hili liweze kutekelezwa haraka?

Name

Ummy Hamisi Nderiananga

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA WAZIRI MKUU, SERA, URATIBU NA BUNGE (MHE. UMMY H. NDERIANANGA): Mheshimiwa Spika, nakushukuru. Napenda kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Deo Kesenyenda Sanga Mbunge wa Makambako kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, kwa kuzingatia majibu yangu niliyoyatoa katika swali la msingi, nimesema kwamba tunaendelea na maandalizi. Na niliarifu Bunge lako Tukufu kwamba sasa tuko katika maboresho ya daftari la kudumu la wapiga kura. Kwa hiyo kipindi kitakapofika Tume itatangaza na Mheshimiwa Deo ataweza kushirikiana na wananchi wenzake katika wilaya na mkoa ili kuleta mapendekezo ambayo wanaona yanafaa kwa ajili ya jambo hilo analoliomba, asante. (Makofi)

Name

Edwin Enosy Swalle

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Lupembe

Primary Question

MHE. DEO K. SANGA aliuliza: - Je ni lini Serikali itaangalia upya mipaka ya kiutawala katika Jimbo la Makambako?

Supplementary Question 2

MHE. EDWIN E. SWALLE: Mheshimiwa Spika, asante sana Halmashauri ya Njombe DC ambayo ni Jimbo la Lupembe lina kata 12; na kata 4 kati ya hizo kata ya Ninga, Ikuna, Kichiwa,

Mtwango na Igongolo ziko halmashauri ya Makambako na Jimbo la Makambako na hii inaleta ugumu sana kwenye utawala wa shughuli za maendeleo.

Je, ni lini Serikali itarudisha kata hizi kwenye Halmashauri ya Njombe DC kwa ajili ya kiutawala?

Name

Ummy Hamisi Nderiananga

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA WAZIRI MKUU, SERA, URATIBU NA BUNGE (MHE. UMMY H. NDERIANANGA): Mheshimiwa Spika, ahsante, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Mbunge kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, kwa kuwa suala hili pia linahusu wenzetu wa upande Ofisi ya Rais-TAMISEMI, na kwa kuwa suala la halmashauri linasimamiwa chini ya Sheria za Serikali ya Mtaa Sura ya 287 na 288 pamoja na mwongozo wa uanzishwaji wa maeneo ya utawala wa mwaka 2014. Ninaomba nimshauri Mheshimiwa Mbunge muendelee kufuata utaratibu wa vigezo na masharti ili kusudi kuweza kukamilisha jambo hilo; kwa kuanzia katika Serikali za vijiji kwenda kwenye DCC kwenda kwenye RCC halafu mkoa mama utatuletea sisi mapendekezo. Ahsante. (Makofi)

Name

Vita Rashid Kawawa

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Namtumbo

Primary Question

MHE. DEO K. SANGA aliuliza: - Je ni lini Serikali itaangalia upya mipaka ya kiutawala katika Jimbo la Makambako?

Supplementary Question 3

MHE. VITA R. KAWAWA: Mheshimiwa Spika, asante sana kwa kuwa na sisi Jimbo la Namtumbo lina ukubwa wa kilomita za mraba 20,375, na ukienda kwenye kata ya mwisho unatembea kilomita 254; na tumeshakaa vikao vya awali vya wilaya na mkoa ili kuweka mapendekezo ya kuomba jimbo letu ligawiwe.

Je, Serikali wakati ukifika inaweza ikatuweka katika orodha ya kugawanywa jimbo hilo?

Name

Ummy Hamisi Nderiananga

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA WAZIRI MKUU, SERA, URATIBU NA BUNGE (MHE. UMMY H. NDERIANANGA): Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Mheshimiwa Waziri Mkuu naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Vita Kawawa Mbunge wa Namtumbo kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, tunatambua kwamba yapo majimbo ni makubwa na sisi tunafahamu. Hata hivyo, kama nilivyojibu katika swali la msingi lililoulizwa na Mheshimiwa Deo napenda nimhakikishie kwamba muda utakapofika na Tume itakapotangaza basi na yeye tutamweka kwenye orodha kwa kuzingatia vigezo na masharti, ahsante. (Makofi)