Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 7 Sitting 16 Policy, Coordination and Parliamentary Affairs Ofisi ya Waziri Mkuu Sera, Uratibu na Bunge 129 2022-05-05

Name

Deo Kasenyenda Sanga

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Makambako

Primary Question

MHE. DEO K. SANGA aliuliza: -

Je ni lini Serikali itaangalia upya mipaka ya kiutawala katika Jimbo la Makambako?

Name

Ummy Hamisi Nderiananga

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA WAZIRI MKUU, SERA, URATIBU NA BUNGE (MHE. UMMY H. NDERIANANGA) alijibu: -

Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Mheshimiwa Waziri Mkuu naomba kujibu swali la Mheshimiwa Deo Kesenyenda Sanga Mbunge wa Makambako kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, kwa mujibu wa Ibara ya 74(6)(c) ya Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ya mwaka 1977, Tume ya Taifa ya Uchaguzi ndiyo yenye dhamana ya kuchunguza mipaka na kuigawa nchi katika majimbo ya uchaguzi kwa ajili ya uchaguzi wa Wabunge.

Mheshimiwa Spika, Katika maandalizi ya kuelekea Uchaguzi Mkuu wa Mwaka 2025, Tume kwa kuzingatia matakwa ya Katiba itatangaza utaratibu na sifa za kugawa maeneo mbalimbali kwa ajili ya uchaguzi. Hivyo, Mheshimiwa Mbunge anashauriwa kuwa pindi Tume itakapotoa tangazo la kuanzisha maeneo mapya ya kiutawala, ashirikiane na Mamlaka za kiutawala katika Wilaya na Mkoa kuandaa na kuwasilisha mapendekezo kwa kuzingatia vigezo vitakavyokuwa vimewekwa na Tume. Ahsante.