Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Asia Abdulkarim Halamga

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. ASIA A. HALAMGA K.n.y. MHE. NG’WASI D. KAMANI aliuliza: - Je, lini Serikali itafupisha muda wa miaka saba kwa elimu ya msingi na sita ya sekondari ili kupunguza muda kwa wanafunzi wenye uwezo mkubwa?

Supplementary Question 1

MHE. ASIA A. HALAMGA: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana. Naomba sasa niulize maswali mawili ya nyongeza.

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa kuwa mwongozo huu ulitoka mwaka 2019 na sasa ni mwaka 2022; je, Serikali imefanya tathmini na kugundua changamoto zipi juu ya mwongozo huo, na nini majibu ya Serikali baada ya kugundua changamoto zilizopo katika mwongozo huo?

Mheshimiwa Naibu Spika, swali langu la pili; ni lini Serikali itakamilisha uandaaji wa Sera mpya ya Elimu ya Sekondari ili kumpunguzia kijana wa Kitanzania mzigo wa kukaa muda mrefu shuleni? Ahsante.

Name

Omary Juma Kipanga

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mafia

Answer

NAIBU WAZIRI WA ELIMU, SAYANSI NA TEKNOLOJIA: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante na naomba kujibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Asia kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, nadhani tunakumbuka Mheshimiwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania tarehe 22 Aprili, 2021 akihutubia Bunge hili tukufu alituagiza Wizara ya Elimu kuweza kufanya mapitio ya sera, sheria pamoja na mitaala yetu.

Mheshimiwa Naibu Spika, zoezi hilo ndilo ambalo linaendelea hivi sasa na katika mapitio haya ya sera, sheria pamoja na mitaala, suala la miongozo hii kufanyiwa tathmini nalo limeingizwa ambapo tutafanya tathmini ya kina kuona namna gani miongozo hii tunaweza kuirekebisha kulingana na wakati.

Mheshimiwa Naibu Spika, katika swali lake la pili, anauliza muda gani tutatumia; naomba nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kuwa mpaka kufika mwaka wa fedha ujao tutakuwa tumekamilisha utaratibu wa mapitio ya sera, sheria pamoja na mitaala hii ili iweze kuanza kutumika. Nakushukuru sana.

Name

Issaay Zacharia Paulo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mbulu Mjini

Primary Question

MHE. ASIA A. HALAMGA K.n.y. MHE. NG’WASI D. KAMANI aliuliza: - Je, lini Serikali itafupisha muda wa miaka saba kwa elimu ya msingi na sita ya sekondari ili kupunguza muda kwa wanafunzi wenye uwezo mkubwa?

Supplementary Question 2

MHE. ZACHARIA P. ISSAAY: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru sana kwa kunipa nafasi niulize swali dogo la nyongeza.

Mheshimiwa Naibu Spika, pamoja na hatua kubwa ya wahitimu nchini wa sekta ya elimu, zaidi ya asilimia 70 ya wahitimu wa vyuo nchini ni walimu.

Je, Serikali haioni kuwa ni wakati mwafaka sasa wa kuhamasisha fani nyingine ili vijana wetu wanapomaliza kidato cha nne waweze kusoma fani nyingine kwa mazingira wezeshi?

Name

Omary Juma Kipanga

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mafia

Answer

NAIBU WAZIRI WA ELIMU, SAYANSI NA TEKNOLOJIA: Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kujibu swali dogo la nyongeza la Mheshimiwa Zacharia Issaay kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, jambo ambalo anazungumza Mheshimiwa Mbunge ni kweli, na kama nilivyojibu kwenye majibu yangu ya msingi, kwa vile sasa tunafanya mapitio ya sera, sheria pamoja na mitaala yetu ambayo tunakwenda kuhakikisha kwamba maeneo mengi ambayo yanabeba fani za ufundi tunakwenda kuyafanyia kazi. Kwa hiyo, nimuondoe wasiwasi katika eneo hilo, kwa vile amesema wengi ni walimu hata huko huko kwenye ualimu nako tukiweka na stadi zlie za kazi tunaweza tukaondoa changamoto hiyo ya ajira.