Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 7 Sitting 17 Education, Science,Technology and Vocational Training, Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia 146 2022-05-06

Name

Ng'wasi Damas Kamani

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. ASIA A. HALAMGA K.n.y. MHE. NG’WASI D. KAMANI aliuliza: -

Je, lini Serikali itafupisha muda wa miaka saba kwa elimu ya msingi na sita ya sekondari ili kupunguza muda kwa wanafunzi wenye uwezo mkubwa?

Name

Omary Juma Kipanga

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mafia

Answer

NAIBU WAZIRI WA ELIMU, SAYANSI NA TEKNOLOJIA alijibu: -

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa niaba ya Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Ng’wasi Damas Kamani, Mbunge wa Viti Maalum, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, suala la miaka inayotumika kumuandaa mhitimu wa elimu ya msingi na sekondari hutegemea kiasi cha maudhui yanayotakiwa kujengwa ili kumuwezesha mhitimu kupata stadi na ujuzi unaohitajika kulingana na mahitaji ya wakati.

Mheshimiwa Naibu Spika, Serikali kwa kutambua uwepo wa wanafunzi wenye uwezo tofauti katika kujifunza mwaka 2019 ilitoa mwongozo kuhusu utaratibu wa kurusha darasa wanafunzi wa elimu ya msingi. Mwongozo huo unatoa utaratibu unaopaswa kufuatwa na uongozi wa shule kwa kushirikiana na mzazi wa mtoto husika katika kumrusha darasa mwanafunzi anayeonekana kuwa na uwezo mkubwa darasani. Aidha, baada ya kufanyika kwa tathmini ya utekelezaji wa mwongozo huo Serikali itaona namna ya kuendelea na utaratibu huo kwa ngazi nyingine za elimu. Nakushukuru sana.