Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Constantine John Kanyasu

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Geita Mjini

Primary Question

MHE. CONSTANTINE J. KANYASU aliuliza: - Je, ni lini Serikali itajenga upya Bwawa la Kasamwa na kutenganisha mwingiliano wa binadamu na mifugo?

Supplementary Question 1

MHE. CONSTANTINE J. KANYASU: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru sana, kwanza naomba nimshukuru Mheshimiwa Waziri kwa ahadi ya kufanya upembuzi yakinifu kwenye mwaka huu wa fedha, lakini Bwawa la Kasamwa pamoja na kuhudumia wananchi limesababisha Kiwanda cha Pamba cha Kasamwa pamoja na Kiwanda cha Mafuta kutofanya kazi kwa sababu hakuna maji. Sasa ni lini baada ya upembuzi yakinifu ujenzi wa bwawa hilo utafanyika?

Mheshimiwa Naibu Spika, la pili, nawapongeza GEUWASA, wanafanya kazi yao ya kusambaza maji vizuri. Lakini maji ya GEUWASA ni ya nyumbani (domestic) na maji ya bwawa yanategemewa kwa ajili ya mifugo na kuna mnada mkubwa pale wa mifugo. Sasa ni lini ujenzi wa bwawa hilo utapewa kipaumbele ili kuokoa mifugo inayokwenda Kasamwa pale? Nakushukuru sana. (Makofi)

Name

Jumaa Hamidu Aweso

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Pangani

Answer

WAZIRI WA MAJI: Mheshimiwa Naibu Spika, kwanza nimtoe hofu Mheshimiwa Constantine Kanyasu, Mbunge wa Geita Mjini, kwa kazi nzuri anayoifanya, lakini nataka nimhakikishie kuwa kupitia Wizara yetu ya Maji tumepata fedha kwa ajili ya kununua mitambo seti tano kwa ajili ya uchimbaji wa mabwawa. Kwa hiyo, moja ya maeneo ambayo tutaweza kuwapa kipaumbele ni eneo katika Jimbo lake la Geita Mjini.

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa hiyo kikubwa, nataka nimhakikishie kuwa mitambo itakapokuwa imefika mwezi huu wa Juni, moja ya maeneo ambayo tutayapa kipaumbele ni eneo la Geita kwa sababu kumekuwa na uhitaji mkubwa sana. Ahsante sana.

Name

Agnes Elias Hokororo

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. CONSTANTINE J. KANYASU aliuliza: - Je, ni lini Serikali itajenga upya Bwawa la Kasamwa na kutenganisha mwingiliano wa binadamu na mifugo?

Supplementary Question 2

MHE. AGNES E. HOKORORO: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante kwa kunipa nafasi niulize swali la nyongeza.

Je, ni lini Serikali itasafisha ili kuongeza kina cha Bwawa la Lukuledi ikiwa ni ahadi yake Mheshimiwa Waziri ya mwaka 2021, maji ambayo yanatumika katika Vijiji vya Lukuledi, Mwangawaleo, Ndomoni, Mraushi na Nambawala?

Name

Jumaa Hamidu Aweso

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Pangani

Answer

WAZIRI WA MAJI: Mheshimiwa Naibu Spika, kwanza nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kuwa moja ya changamoto kubwa katika utekelezaji wa mabwawa ilikuwa suala zima la vifaa. Lakini tumekwishapata fedha juu ya ununuzi wa vifaa hivi vya kisasa na moja ya maeneo ambayo tutayapa nguvu na ya kipaumbele ni kuhakikisha kwamba tunajenga mabwawa. Kwa hiyo, tutawapa kipaumbele katika kuhakikisha mabwawa ambayo yatakayokuwa yamejengwa na yeye jimboni kwake.

Name

Furaha Ntengo Matondo

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. CONSTANTINE J. KANYASU aliuliza: - Je, ni lini Serikali itajenga upya Bwawa la Kasamwa na kutenganisha mwingiliano wa binadamu na mifugo?

Supplementary Question 3

MHE. FURAHA N. MATONDO: Mheshimiwa Naibu Spika, nashukuru sana kwa kunipa nafasi.

Mheshimiwa Naibu Spika, Mkoa wa Mwanza tumekuwa na shida sana na kero ya maji, na hasa miradi ambayo haitekelezeki, na ukizingatia Mwanza tumezungukwa na ziwa.

Je, ni lini Serikali itatekeleza miradi ya maji katika Mkoa wa Mwanza tukaondokana na kero ambayo inatukumba mpaka muda huu?

Name

Jumaa Hamidu Aweso

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Pangani

Answer

WAZIRI WA MAJI: Mheshimiwa Naibu Spika, nikiri katika Jiji la Mwanza pamoja na mradi tuliokuwa nao lakini ongezeko la watu limesababisha uhitaji mkubwa wa maji. Tuna mradi sasa hivi tunaongeza chanzo katika eneo la Butimba ili kuongeza uzalishaji na wananchi hawa waweze kupata huduma ya maji safi na salama. Tumepata fedha zaidi ya shilingi bilioni 65 katika kuhakikisha kazi ile inaanza na mkandarasi yuko site.

Mheshimiwa Naibu Spika, kubwa sisi kama Wizara ya Maji tutausimamia na kuufuatilia mradi ule ukakamilike kwa wakati ili uweze kuongeza uzalishaji na wananchi wa Jiji la Mwanza kwa maana ya Ilemela pamoja na Nyamagana kuweza kupata huduma ya maji safi na salama. (Makofi)

Name

Dr. John Danielson Pallangyo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Arumeru-Mashariki

Primary Question

MHE. CONSTANTINE J. KANYASU aliuliza: - Je, ni lini Serikali itajenga upya Bwawa la Kasamwa na kutenganisha mwingiliano wa binadamu na mifugo?

Supplementary Question 4

MHE. DKT. JOHN D. PALLANGYO: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru kwa kunipa nafasi na mimi na kwanza nitoe shukrani zangu za dhati kwa Mheshimiwa Waziri ambaye wakati alipokuwa jimboni kwangu mara ya mwisho alitoa maelekezo ya namna ya kutatua changamoto ya mafuriko yanayosababishwa na kufukiwa korongo la Mto Nduruma na kutesa wananchi wa Kata za Shambarai Burka, Mbuguni, Majengo na Makiba.

Mheshimiwa Naibu Spika, lakini baada ya ziara ya wale wataalam ambao walitumwa...

NAIBU SPIKA: Mheshimiwa Pallangyo swali.

MHE. DKT. JOHN D. PALLANGYO: ...kimya kimetanda. Swali sasa, je, Serikali ina mkakati gani wa kutenga fedha kwa ajili ya kwenda kutatua ile changamoto ya mafuriko?

Name

Jumaa Hamidu Aweso

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Pangani

Answer

WAZIRI WA MAJI: Mheshimiwa Naibu Spika, ni kweli nimefanya ziara katika Jimbo la Mheshimiwa Mbunge la Arumeru Mashariki na moja ya ahadi ni kuwapatia fedha.

Mheshimiwa Naibu Spika, nimeshatoa fedha mwezi huu, shilingi milioni 100, kwa ajili ya uanzaji wa kazi ile. Mheshimiwa Mbunge unaweza ukafuatilia katika hilo. (Makofi)