Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 7 Sitting 17 Water and Irrigation Wizara ya Maji 145 2022-05-06

Name

Constantine John Kanyasu

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Geita Mjini

Primary Question

MHE. CONSTANTINE J. KANYASU aliuliza: -

Je, ni lini Serikali itajenga upya Bwawa la Kasamwa na kutenganisha mwingiliano wa binadamu na mifugo?

Name

Jumaa Hamidu Aweso

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Pangani

Answer

WAZIRI WA MAJI alijibu: -

Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Constantine John Kanyasu, Mbunge wa Jimbo la Geita Mjini, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, Bwawa la Kasamwa lilijengwa kwa ajili ya shughuli mbalimbali za kijamii ikiwemo kutoa huduma za maji kwa ajili ya matumizi ya binadamu, viwanda, kunyweshea mifugo pamoja na kilimo.

Mheshimiwa Naibu Spika, katika mwaka wa fedha 2022/2023 Serikali itafanya usanifu kwa ajili ya kukarabati bwawa hilo ambapo pia itajumuisha miundombinu kwa ajili ya kunyweshea mifugo.