Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Sebastian Simon Kapufi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mpanda Mjini

Primary Question

MHE. SEBASTIAN S. KAPUFI aliuliza: - Je, Serikali ina mpango gani wa kuongeza watumishi katika Manispaa ya Mpanda hasa katika maeneo ya afya, elimu na maendeleo ya jamii?

Supplementary Question 1

MHE. SEBASTIAN S. KAPUFI: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru, ninayo maswali mawili ya nyongeza.

Kwa bahati mbaye, Manispaa ya Mpanda ni kati ya Manispaa zilizopo pembezoni, mwaka jana tulipata walimu sita na watumishi wa afya saba. Serikali inasema nini katika kuinusuru Halmashauri hii na upungufu wa watumishi?

Mheshimiwa Naibu Spika, swali la pili, wamekuwepo watu ambao wamekuwa wakijitolea kwa muda mrefu bila kuathiri taratibu za ajira, Serikali inasema nini katika kuajiri watu hawa ambao wamekuwa wakijitolea?

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE): Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kujibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Sebastian Simon Kapufi, Mbunge wa Jimbo la Mpanda Mjini kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, kwanza nianze kwa kumpongeza sana Mheshimiwa Kapufi kwa kazi kubwa na nzuri anayoifanya kwa kuwasemea Wananchi wa Mpanda Mjini na nimhakikishie kwamba Ofisi ya Rais, TAMISEMI tutaendelea kushirikiana kwa karibu sana.

Mheshimiwa Naibu Spika, lakini nimhakikishie kwamba tunajua mwaka uliopita walipata watumishi hawa sita wa elimu na saba wa afya lakini ukiangalia asilimia ya watumishi kwa Mpanda ni asilimia 69.1 angalia kidogo ukilinganisha na Halmashauri nyingine. Lakini hii haimaanishi kwamba hatutaleta watumishi na ndio maana kwenye ajira hizi za mwaka huu bado Mpanda itapata kipaumbele.

Mheshimiwa Naibu Spika, lakini pili kwa watumishi wanaojitolea Serikali imeweka utaratibu wa kuwapa kipaumbele watumishi wale ambao wanajitolea kwenye vituo vyetu na shule zetu ili ajira zinapotokea waweze kupata ajira kuwa kipaumbele zaidi, ahsante.

Name

Minza Simon Mjika

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. SEBASTIAN S. KAPUFI aliuliza: - Je, Serikali ina mpango gani wa kuongeza watumishi katika Manispaa ya Mpanda hasa katika maeneo ya afya, elimu na maendeleo ya jamii?

Supplementary Question 2

MHE. MINZA S. MJIKA: Mhesimiwa Naibu Spika, nashukuru kwa kuniona, naomba niulize swali la nyongeza, je, ni lini Serikali itaongeza watumishi wa afya katika Wilaya ya Meatu?

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE): Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Minza, Mbunge wa Viti Maalum kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, nafahamu kwamba Halmashauri ya Meatu ina upungufu wa watumishi na itapewa kipaumbele kwenye ajira hizi ambazo zimekwishatangazwa.

Name

Joseph Michael Mkundi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ukerewe

Primary Question

MHE. SEBASTIAN S. KAPUFI aliuliza: - Je, Serikali ina mpango gani wa kuongeza watumishi katika Manispaa ya Mpanda hasa katika maeneo ya afya, elimu na maendeleo ya jamii?

Supplementary Question 3

MHE. JOSEPH M. MKUNDI: Mheshimiwa Naibu Spika, nashukuru, Halmashauri ya Wilaya ya Ukerewe ina upungufu wa watumishi kada ya ualimu zaidi ya 1,700 ambayo ni karibu asilimia 40 na watumishi karibu 170 ambao ni karibu asilimia 56 kwenye kada ya afya. Je, Serikali iko tayari sasa kwenye ajira zinazokuja hivi karibuni kutoa kipaumbele kwenye Halmashauri ya Wilaya ya Ukerewe? Nakushukuru.

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE): Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Mkundi, Mbunge wa Jimbo la Ukerewe kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, Serikali imefanya tathimini kuona maeneo yenye upungufu mkubwa zaidi wa watumishi wa elimu, afya na watumishi wa kada nyingine ikiwemo Ukerewe na maeneo haya ndiyo yatakayopewa kipaumbele cha juu zaidi kuliko yale maeneo ambayo yana watumishi wa kutosha. Kwa hiyo, Mheshimiwa Mbunge tutatoa kipaumbele Ukerewe, ahsante.

Name

Sophia Hebron Mwakagenda

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. SEBASTIAN S. KAPUFI aliuliza: - Je, Serikali ina mpango gani wa kuongeza watumishi katika Manispaa ya Mpanda hasa katika maeneo ya afya, elimu na maendeleo ya jamii?

Supplementary Question 4

MHE. SOPHIA H. MWAKAGENDA: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana, kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali la nyongeza.

Mheshimiwa Waziri ajira mlizotangaza, hakuna option inaonesha wale waliojitolea muda mrefu, mnaweza mkawatambua na kuweza kuwasaidia katika kuwachagua. Ni nini Serikali mtafanya kuhakikisha hao wanaojitolea wanapewa kipaumbele cha kwanza na wengine wanafuata? Ahsante. (Makofi)

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE): Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Sophia Mwakagenda, Mbunge wa Viti Maalum kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, tunaweka utaratibu wa kutoa matangazo kwa ajili ya ajira za watumishi, lakini naomba Mheshimiwa Naibu Spika, Bunge lako tukufu lifahamu kwamba pamoja na watumishi ambao wanajitolea, si watumishi wote waliomaliza vyuo wanaomba kujitolea wanapata nafasi ya kujitolea. Kwa hiyo, bado kuna changamoto ya wale wanaokubaliwa kupata nafasi ya kujitolea. Kwa hiyo, tukiweka kujitolea ya kwamba ni absolute criteria maana yake kuna wale ambao walikuwa na nia ya kujitolea, lakini walioomba hawakupata, watakosa nafasi ya kuajiriwa.

Mheshimiwa Naibu Spika, na ndiyo tunakwenda kwa utaratibu kwamba tunawapa kipaumbele kwa sababu wanajitolea na Wakurugenzi sasa wanatupa orodha ya watumishi waliokuwa wanajitolea kupitia Halmashauri zetu, lakini na sisi hata ambao hawajajitolea tunawapa criteria ya priority kwa sababu wako walioomba na hawakufanikiwa kupata nafasi hiyo, ahsante.