Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Rashid Abdallah Shangazi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mlalo

Primary Question

MHE. RASHID A. SHANGAZI K.n.y. MHE. KENETH E. NOLLO aliuliza: - Je, Serikali ina mpango gani wa kujenga daraja la kudumu kwenye Mto Mzizima ili barabara ya Kigwe hadi Chipanga Wilayani Bahi iweze kupitika mwaka mzima?

Supplementary Question 1

MHE. RASHID A. SHANGAZI: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante kwa majibu mazuri ya Serikali yenye matumaini kwa wananchi wa Jimbo la Bahi, lakini nina swali moja la nyongeza.

Mheshimiwa Naibu Spika, kule Kata ya Mwangoi na Kata ya Dule Mlalo ambako linaunganishwa na Mto Umba, mto ule umehama na kusababisha kina cha maji kushuka chini zaidi na hivyo daraja limezama katika eneo lile, lakini Ofisi ya Rais, TAMISEMI kupitia TARURA wameshafanya tathmini.

Sasa nauliza ni lini ujenzi wa daraja jipya linalounganisha Kata ya Mwangoi na Kata ya Dule katika Kijiji cha Chamlesa litaanza?

Name

David Ernest Silinde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tunduma

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DAVID E. SILINDE): Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kujibu swali dogo la nyongeza la Mheshimiwa Rashid Shangazi, Mbunge wa Mlalo kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, barabara ambayo ameianisha pamoja na hilo eneo ambalo daraja linahitajika, kati ya Mwongoi na Dule, daraja hilo lipo katika mpango na tutalitekeleza katika mwaka wa fedha 2022/2023 yaani mwaka unaofuatia.

Name

Japhet Ngailonga Hasunga (CPA)

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Vwawa

Primary Question

MHE. RASHID A. SHANGAZI K.n.y. MHE. KENETH E. NOLLO aliuliza: - Je, Serikali ina mpango gani wa kujenga daraja la kudumu kwenye Mto Mzizima ili barabara ya Kigwe hadi Chipanga Wilayani Bahi iweze kupitika mwaka mzima?

Supplementary Question 2

MHE. JAPHET N. HASUNGA: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana, katika Kata ya Isalalo kwenda kwenye Kata ya Ikunga, kuna mto mkubwa wa Nkana.

Je, Serikali ina mpango gani ili kuwafanya wananchi wa Isalalo waweze kuvuka kwenda Kata ya Ipunga kwenye Kijiji cha Ipanzya?

Name

David Ernest Silinde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tunduma

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DAVID E. SILINDE): Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Japhet Hasunga, Mbunge wa Jimbo la Vwawa kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, bahati nzuri eneo ambalo amelianisha Mheshimiwa Mbunge ninalifahamu na bahati nzuri niko huko huko katika Halmashauri ya Wilaya ya Mbozi, nimhakikishie tu Mheshimiwa Mbunge kwamba tumeshawaagiza watu wa TARURA Mkoa wa Songwe waende wakafanye tathmini katika eneo hilo ili watupe tathmini ili tutafute fedha kwa ajili ya ujenzi wa daraja katika eneo hilo.

Name

Bonnah Ladislaus Kamoli

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Segerea

Primary Question

MHE. RASHID A. SHANGAZI K.n.y. MHE. KENETH E. NOLLO aliuliza: - Je, Serikali ina mpango gani wa kujenga daraja la kudumu kwenye Mto Mzizima ili barabara ya Kigwe hadi Chipanga Wilayani Bahi iweze kupitika mwaka mzima?

Supplementary Question 3

MHE. BONNAH L. KAMOLI: Mheshimiwa Naibu Spika, nashukuru, naomba kumuuliza Mheshimiwa Waziri, Serikali ina mpango gani na barabara ya Kisukulu - Maji Chumvi ambayo imeharibika sana sasa hivi na wananchi hawawezi kupita?

Name

David Ernest Silinde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tunduma

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DAVID E. SILINDE): Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana na naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Bonnah Kamoli, Mbunge wa Segerea kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, barabara hii ambayo ameianisha Mheshimiwa Mbunge inafanyiwa tathmini kwa wakati wa sasa na watakapomaliza tathmini tutampatia taarifa Mheshimiwa Mbunge, ni lini sasa tunaanza rasmi ujenzi katika eneo hilo.