Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 7 Sitting 17 Regional Administration and Local Government Authorities Ofisi ya Rais TAMISEMI. 139 2022-05-06

Name

Kenneth Ernest Nollo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bahi

Primary Question

MHE. RASHID A. SHANGAZI K.n.y. MHE. KENETH E. NOLLO aliuliza: -

Je, Serikali ina mpango gani wa kujenga daraja la kudumu kwenye Mto Mzizima ili barabara ya Kigwe hadi Chipanga Wilayani Bahi iweze kupitika mwaka mzima?

Name

David Ernest Silinde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tunduma

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DAVID E. SILINDE) alijibu: -

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa niaba ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, TAMISEMI naomba kujibu swali la Mheshimiwa Kenneth Nollo, Mbunge wa Bahi kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, katika mwaka wa fedha 2021/2022 Serikali kupitia TARURA Wilaya ya Bahi, imetenga fedha kiasi cha shilingi milioni 620.23 kwa ajili ya ujenzi wa daraja (box culvert) lenye urefu wa mita 34. Ujenzi wa daraja hili umeanza tarehe 20 Februari, 2022 na unatarajiwa kukamilika tarehe 19 Agosti, 2022 na ujenzi wa mradi huu umefikia asilimia 30. Kazi hiyo inafanywa na Mkandarasi Ravji Construction Ltd.

Mheshimiwa Naibu Spika, kukamilika kwa ujenzi wa daraja hilo utaifanya barabara ya Kigwe – Chipanga kupitika wakati wote na hivyo kuondoa kero ya wananchi kutumia muda mwingi wa kusubiria maji ya mto yapungue ili wavuke na kuendelea na shughuli za kiuchumi na kijamii.