Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Angelina Adam Malembeka

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. ANGELINA ADAM MALEMBEKA aliuliza: - Je, ukaguzi wa magari barabarani unahusisha vitu gani?

Supplementary Question 1

MHE. ANGELINA ADAM MALEMBEKA: Mheshimiwa Spika, ahsante sana kwa kunipa fursa ya kuuliza maswali mawili ya nyongeza. Kwanza nimpongeze Mheshimiwa Naibu Waziri kwa majibu mazuri yenye ufasaha zaidi, lakini nina maswali mawili ya nyongeza. Swali la kwanza, katika majibu yake ameelezea uwezo wa gari pia uzima na usalama wa gari. Sasa hivi kuna magari mengi yanayobeba vinywaji baridi kusambaza madukani kumekuwa na utaratibu wa makusudi kuyapanua na kuyatanua magari yale kiasi kwamba hata dereva inabidi aweke nondo ili aweze kuipata ile site mirror vizuri. Je, Serikali ina kauli gani kuhusiana wamiliki wa magari hayo ambao wanapanua kwa makusudi magari hayo? (Makofi)

Mheshimiwa Spika, swali langu la pili kwa kuwa pia ameelezea uzima na usalama wa magari, tuna magari mengi yanayobeba takataka lakini magari yale yenyewe ni sehemu ya takataka. Kama ni kweli yanakaguliwa kuangalia uzima wake na usalama, Serikali ina kauli gani kuhusiana na magari yanayobeba takataka ambayo yenyewe pia ni takataka? Ahsante. (Makofi)

Name

Sagini Jumanne Abdallah

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Butiama

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI: Mheshimiwa Spika, naomba kujibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Malembeka, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, moja kuhusu magari ya vinywaji baridi kupanuliwa kwa maana ya kuzidi uwezo wake wa kawaida, nadhani hili ni suala ambalo ni la viwango, tutashauriana na Wizara yenye dhamana ya Uchukuzi, na Wizara yenye dhamana ya Viwanda hili wanapokagua kwa maana ya TBS, magari yanavyoingia basi yazingatie uwezo na sura ya gari, sio ya upanuzi ambao unaathiri watumiaji wengine wa magari, kama alivyoeleza inatanuliwa mpaka site mirror zinaongezwa kiasi ambacho kinaleta usumbufu, ili watakapotoa viwango vile basi askari wetu wa usalama barabarani wanapotimiza wajibu wao wa kuona magari yanayostahili kuwa barabarani basi watasimamia kwa mujibu wa miongozo hiyo.

Mheshimiwa Spika, kuhusu magari ya taka, ambayo amesema yenyewe ni takataka, nadhani nizielekeze mamlaka zinazoyaajiri magari haya kwa Mamlaka za Miji na Majini, wahakikishe kwamba wanateuwa wakandarasi wenye uwezo wa kutoa magari yanayofaa badala ya magari haya ya kubeba taka yenyewe yanakuwa sehemu ya uchafuzi wa miji yetu. Nashukuru.