Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 7 Sitting 15 Home Affairs Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi 127 2022-04-29

Name

Angelina Adam Malembeka

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. ANGELINA ADAM MALEMBEKA aliuliza: -

Je, ukaguzi wa magari barabarani unahusisha vitu gani?

Name

Sagini Jumanne Abdallah

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Butiama

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI alijibu: -

Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, napenda kujibu swali na Mheshimiwa Angelina Adam Malembeka, Mbunge wa Viti Maalum, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, Ukaguzi wa magari hufanywa kwa mujibu wa Sheria ya Usalama Barabarani, Sura ya 168 ya mwaka 1973 kama ilivyofanyiwa marejeo mwaka 2002 na kanuni zake. Ukaguzi wa magari uko wa aina mbili, aina ya kwanza hufanywa kwa mujibu wa Kifungu cha 81 ambao ni ukaguzi wa kawaida unaofanywa na askari barabarani. Ukaguzi huu huangalia nyaraka za gari, leseni ya dereva, uwezo wa gari, madai ya tozo za faini, pamoja na hali ya dereva.

Mheshimiwa Spika, aina ya pili ya ukaguzi hufanywa kwa mujibu wa Kifungu cha 83 ambapo Mkaguzi wa Magari hufanya ukaguzi kwenye maeneo maalum na baada ya kukagua hutoa hati ya ukaguzi kwa maana ya PF 93. Ukaguzi huu wa magari hufanywa ili kujiridhisha na uzima na usalama wa gari kama vile mifumo ya breki, umeme, sterling, matairi na kadhalika. Nashukuru.