Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Flatei Gregory Massay

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mbulu Vijijini

Primary Question

MHE. FLATEI G. MASSAY aliuliza: - Je, ni lini Serikali itatekeleza ahadi yake ya kujenga mabwawa katika Jimbo la Mbulu Vijijini?

Supplementary Question 1

MHE. FLATEI G. MASSAY: Mheshimiwa Spika, ahsante kwa kunipa nafasi ya kuuliza maswali mawili ya nyongeza.

Mheshimiwa Spika, kwa kuwa mabwawa ambayo yanajengwa na tumeleta kwenye Wizara yako, Bwawa la Mungahai, Dirimu, Yaeda Chini, Masieda, Endagichani, Basodere, Eshdeshi, Getire na Haribapeti.

Je, ni lini unatujengea mabwawa haya ambayo tumeshayaleta kwenye Wizara yako?

Mheshimiwa Spika, swali la pili kwa kuwa Waziri alikuja Haydom na akaahidi kwamba tusubiri wali wa kushiba unaonekana mezani, na akaahidi kisima cha Haydom.

Je, ni lini kinachimbwa?

Name

Maryprisca Winfred Mahundi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAJI: Mheshimiwa Spika, ahsante. Naomba kujibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Massay kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, kuhusiana na mabwawa, mabwawa haya yapo katika ngazi mbalimbali za utekelezaji na maeneo mengi ya nchi tunafikiria kuchimba mabwawa kwa lengo la kuhifadhi maji ya mvua kutumika wakati wa kiangazi, hivyo mwaka ujao wa fedha naamini maeneo kadhaa yatapata huduma hii.

Mheshimiwa Spika, swali la pili kuhusiana na kisima alichokiahidi Mheshimiwa Waziri, ahadi ni deni lazima tutakuja kuchimba hiki kisima, tutaangalia bajeti hii kabla haijakamilika mwaka huu wa fedha na ikibidi basi mwaka ujao wa fedha kisima hiki kitapatikana. (Makofi)