Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 7 Sitting 15 Water and Irrigation Wizara ya Maji 125 2022-04-29

Name

Flatei Gregory Massay

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mbulu Vijijini

Primary Question

MHE. FLATEI G. MASSAY aliuliza: -

Je, ni lini Serikali itatekeleza ahadi yake ya kujenga mabwawa katika Jimbo la Mbulu Vijijini?

Name

Maryprisca Winfred Mahundi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAJI alijibu: -

Mheshimiwa Spika, ahsante. Kwa niaba ya Waziri wa Maji naomba kujibu swali la Mheshimiwa Flatei Gregory Massay, Mbunge wa Jimbo la Mbulu Vijijini, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, Serikali imeendelea kutekeleza miradi ya maji katika Wilaya ya Mbulu Vijijini kwa lengo la kuboresha huduma ya upatikanaji wa maji. Katika Mwaka wa Fedha 2021/2022, ujenzi wa miradi ya maji ya visima virefu kwenye vijiji vya Ng’orati, Maretadu Juu, Labay, Genda, Masqaroda, Mewadani, miradi ya maji ya Singu na ukarabati wa visima katika vijiji vya Domanga, Eshkesh unaendelea. Miradi hiyo itakamilika Septemba, 2022 na itaboresha huduma ya maji katika Wilaya ya Mbulu Vijijini kutoka asilimia 61 hadi kufikia asilimia 76 ifikapo Desemba, 2022.

Mheshimiwa Spika, ujenzi wa mabwawa hasa katika maeneo kame unalenga kukusanya maji yaweze kutumika wakati wa kiangazi ili kuhakikisha shughuli za kilimo na ufugaji zinaimarika.

Katika mwaka wa fedha 2022/2023, Serikali itaendelea kuainisha maeneo ya ujenzi wa malambo na mabwawa madogo katika Wilaya ya Mbulu Vijijini ili kukusanya maji kwa ajili ya shughuli za kiuchumi.