Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Fakharia Shomar Khamis

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. FAKHARIA SHOMAR KHAMIS aliuliza: - Je, Serikali haioni umuhimu wa kutoa nakala ya Sheria ya Maadili kwa Viongozi nchini ikiwemo Wabunge na Viongozi wengine ili kuepuka kukiuka Sheria hiyo?

Supplementary Question 1

MHE. FAKHARIA SHOMAR KHAMIS: Mheshimiwa Spika, kwanza nimshukuru Mheshimiwa Waziri kwa kujibu kwa ufasaha na umejibu vizuri kwa kweli. Lakini nitakuwa na maswali mawili ya nyongeza. Kwa kuwa ofisi ya maadili ni ofisi ya muungano lazima itakuwa na wafanyakazi wa muungano waliokuwepo Zanzibar nao pia wanahusika.

Je, katika hii warsha na makongamano na semina ambazo unazitoa, kwa upande wa wafanyakazi waliokuwepo Zanzibar, nao pia wamepatiwa?

Mheshimiwa Spika, swali la pili, kwa kuwa unahitajika lazima ofisi yako iwe na mjengo Zanzibar wa kufanyia kazi.

Je, ofisi yako unayofanyia kazi kwa Zanzibar iko sehemu gani kazi?

Name

Deogratius John Ndejembi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chamwino

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, MENJIMENTI YA UTUMISHI WA UMMA NA UTAWALA BORA: Mheshimiwa Spika, naomba kujibu maswali mawili ya Mheshimiwa Fakharia Shomar Khamisi kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, kama nilivyosema kwenye majibu yangu ya msingi, kwamba viongozi wote wa Tanzania na Tanzania Zanzibar wamepewa semina hizi na kufanyiwa warsha mbalimbali na makongamano mbalimbali. Kati ya mwaka 2015 hadi 2022 jumla ya viongozi 28,450 wa pande zote mbili za Taifa letu wamefanyiwa semina hizi na warsha hizi wakiwemo Waheshimiwa Wabunge.

Kwa hiyo, nimtoe hofu Mheshimiwa Mbunge, kwamba tutaendelea kutoa warsha hizi na semina hizi kwa waheshimiwa na viongozi wengine mbalimbali ili wote tuweze kuwa na uelewa mmoja kuhusiana na masuala ya maadili.

Mheshimiwa Spika, nikienda kwenye swali lake la pili, ofisi za maadili zipo kila mahali, kila kanda, kila mkoa. Kwa hiyo, hata upande Zanzibar ofisi hizi za maadili zipo katika kila mkoa. Ndiyo maana hata fomu zetu zile tunazozijaza za maadili tuna uwezo wa kuzirudisha katika ofisi zetu hizi zilizo maeneo mbalimbali ya Taifa letu. Naomba kuwasilisha.