Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 7 Sitting 15 Public Service Management Ofisi ya Rais (Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora) 121 2022-04-29

Name

Fakharia Shomar Khamis

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. FAKHARIA SHOMAR KHAMIS aliuliza: -

Je, Serikali haioni umuhimu wa kutoa nakala ya Sheria ya Maadili kwa Viongozi nchini ikiwemo Wabunge na Viongozi wengine ili kuepuka kukiuka Sheria hiyo?

Name

Deogratius John Ndejembi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chamwino

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, MENJIMENTI YA UTUMISHI WA UMMA NA UTAWALA BORA alijibu: -

Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora ninaomba kujibu swali la Mheshimiwa Fakharia Shomar Khamisi (VITI MAALUM) kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika; Serikali imekuwa ikitoa nakala za Sheria ya Maadili ya Viongozi wa Umma Na. 13 ya Mwaka 1995 kwa Viongozi. Serikali hutoa nakala hizo kupitia mikutano, warsha, semina, makongamano na maonyesho mbalimbali. Kati ya mwaka 2015 hadi 2022 Jumla ya nakala 12,400 za Sheria zilichapishwa na kutolewa kwa Viongozi na wadau wengine. Aidha, nakala tepe (soft copy) ya Sheria imewekwa katika tovuti ya Sekretarieti ya Maadili ya Viongozi wa Umma ambayo ni www.ethicssecretariat.go.tz. Hivyo, Viongozi wa Umma wakiwemo Waheshimiwa Wabunge wanashauriwa kutembelea tovuti na kupata nakala ya Sheria.