Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Esther Nicholus Matiko

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. ESTHER N. MATIKO aliuliza: - Je, ni kwa nini Serikali imeshindwa kukamilisha ujenzi wa soko la kimkakati la Kimataifa la Remagwe?

Supplementary Question 1

MHE. ESTHER N. MATIKO: Mheshimiwa Spika, nakushukuru. Kwanza naomba ku-register masikitiko yangu kwa majibu waliyoyatoa Serikali.

Mheshimiwa Spika, tumekuwa tukishuhudia Serikali inakuwa na miradi ambayo haina mpango mkakati madhubuti ya kuonesha ukomo wa mradi. Mathalani hili Soko la Remagwe limetelekezwa tangu Awamu ya Nne, takribani miaka 10.

Je, ni kwa nini Serikali kwa takribani miaka 10 haikuweza kuwa inatenga walau bajeti kila mwaka ili kuhakikisha kwamba inakamilisha huu mradi ambao inakiri kwamba ni wa kimkakati? (Makofi)

Mheshimiwa Spika, swali la pili; Mkoa wa Mara unazalisha mazao ya kibiashara na ya chakula pamoja na mifugo ambapo hulisha ndani ya nchi lakini pia huenda kuuza nchi jirani ya Kenya, ambapo wakulima hawa wanauza kwa bei ‘chee’ baada ya kuwa wameishiwa na muda.

Ni kwa nini sasa Serikali isione umuhimu wa dharura wa kukamilisha soko hili la kimkakati la Kimaitaifa la Remagwe ili kutatua changamoto ya kimasoko kwa wakulima? (Makofi)

Name

Exaud Silaoneka Kigahe

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mufindi Kaskazini

Answer

NAIBU WA UWEKEZAJI, VIWANDA NA BIASHARA: Mheshimiwa Spika, naomba kujibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Esther Matiko, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, kwanza nimshukuru kwa maswali hayo pia niwashukuru Wabunge wa kutoka Tarime, Mheshimiwa Mwita Waitara na Mheshimiwa Michael Kembaki ambao wamekuwa wakifuatilia sana maendeleo ya ujenzi wa soko hilo. Kama nilivyosema Serikali inajua umuhimu wa masoko haya na ndiyo maana tulianza kujenga katika mipaka yote ambayo ni masoko ya kimkakati. Serikali inaendelea kutafuta fedha kama nilivyosema ilikuwa chini ya ufadhili wa benki, ufadhili huo uliisha, kwa hiyo tunatafuta fedha nyingine zaidi ili tukamilishe kujenga majengo hayo.

Mheshimiwa Spika, zaidi tumeshawaambia wenzetu katika Halmashauri kuanza kutenga fedha kidogo kidogo katika bajeti zao kutokana na umuhimu wa masoko haya, kwa hiyo wanachokisema ndiyo Serikali inachokifanya na tunaendelea kufanya hivyo lakini kwasababu ni masoko ya kimkakati yana miundombinu muhimu, kwa hiyo ni lazima tupate fedha za kutosha ili tunapokuja kurudia sasa tukamilishe kwa pamoja kuhakikisha masoko haya yanakamilika katika viwango vinayotakiwa. Nakushukuru.