Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 7 Sitting 13 Industries and Trade Wizara ya Uwekezaji, Viwanda na Biashara 105 2022-04-27

Name

Esther Nicholus Matiko

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. ESTHER N. MATIKO aliuliza: -

Je, ni kwa nini Serikali imeshindwa kukamilisha ujenzi wa soko la kimkakati la Kimataifa la Remagwe?

Name

Exaud Silaoneka Kigahe

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mufindi Kaskazini

Answer

NAIBU WAZIRI WA UWEKEZAJI, VIWANDA NA BIASHARA alijibu: -

Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Uwekezaji, Viwanda na Biashara, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Esther Nicholas Matiko, Mbunge wa Viti Maalum, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, Serikali inatambua umuhimu wa kuwa na masoko ya Kimkakati kwa ajili ya kukuza biashara na mauzo nje ya nchi, kwa maendeleo na ustawi wa wananchi wake.

Mheshimiwa Spika, Serikali iliamua kuanzisha masoko ya kimkakati ya Kimataifa ikiwa ni pamoja na ujenzi wa soko la Remagwe katika mpaka wa Sirari chini ya Mradi wa Uwekezaji wa Sekta ya Kilimo Wilayani, District Agricultural Sector Investment Project (DASIP) uliokuwa unafadhiliwa na Benki ya Maendeleo ya Afrika (AfDB). Serikali inaendelea kutafuta fedha ili kukamilisha ujenzi wa soko hilo.

Mheshimiwa Spika, ninakushukuru.