Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Deodatus Philip Mwanyika

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Njombe Mjini

Primary Question

MHE. DEODATUS P. MWANYIKA aliuliza: - Je, lini Serikali itaanzisha Wakala wa kudhibiti Mazao ya Mbogamboga na Matunda nchini?

Supplementary Question 1

MHE. DEODATUS P. MWANYIKA: Mheshimiwa Spika, ahsante.

Mheshimiwa Spika, kwa sababu ya udharura na kwa ruksa yako naomba kwanza niwape pole wananchi wa Njombe kwa ajali kubwa iliyotokea na iliyouwa watu nane siku ya juzi.

Mheshimiwa Spika, nina maswali mawili madogo ya nyongeza. Swali la kwanza, kwa kuwa suala la gharama na hasa zao la Parachichi lina ushindani mkubwa sana kwenye soko, na suala la gharama ni suala la muhimu sana kuzingatiwa kwa maana ya kupunguza gharama hizo.

Je, Serikali itatuhakikishiaje kwamba mamlaka hii inayoenda kuundwa haitaongeza gharama kwa wakulima wadogo kwa kupitia tozo na gharama za uendeshaji?

Mheshimiwa Spika, swali la pili; Je, ni lini sasa hayo mabadiliko yatafanyika kwa kuletwa Muswada hapa ndani. (Makofi)

Name

Anthony Peter Mavunde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Dodoma mjini

Answer

NAIBU WAZIRI WA KILIMO: Mheshimiwa Spika, napenda kujibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Deodatus Phillip Mwajika Mbunge wa Njombe Mjini kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, ni dhamira ya Serikali kuhakikisha kwamba inakuza tasnia hii ya mazao ya mbogomboga na mazao ya bustani na hivyo moja kati ya maeneo makubwa ambayo tutayasimamia ni kuhakikisha kwamba mkulima hapati changamoto kubwa ya tozo nyingi ambazo zitamfanya akate tamaa ya kilimo chake.

Mheshimiwa Spika, nimuondoe hofu Mheshimiwa Mbunge ya kwamba Serikali katika uanzishwaji wa mamlaka hii itahakikisha kwamba inalinda maslahi ya mkulima na mkulima anufaike na kilimo chake.

Mheshimiwa Spika, pili kuhusu ni lini tutaleta mabadiliko haya ya sheria, mchakato umeshaanza ndani ya Wizara ya kuanza kupitia marekebisho haya ya sheria na pindi itakapokamilika kwa mujibu wa taratibu za Bunge utawasilishwa hapa Bungeni kwa ajili ya majadiliano na kupitishwa.