Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 7 Sitting 13 Livestock , Fisheries, Agriculture, Food Security and Cooperatives Wizara ya Kilimo 103 2022-04-27

Name

Deodatus Philip Mwanyika

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Njombe Mjini

Primary Question

MHE. DEODATUS P. MWANYIKA aliuliza: -

Je, lini Serikali itaanzisha Wakala wa kudhibiti Mazao ya Mbogamboga na Matunda nchini?

Name

Anthony Peter Mavunde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Dodoma mjini

Answer

NAIBU WAZIRI WA KILIMO alijibu: -

Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Kilimo naomba kujibu swali la Mheshimiwa, Deodatus Phillip Mwanyika, Mbunge wa Njombe Mjini, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, Serikali inatambua umuhimu mkubwa wa kuwa na Mamlaka ya kusimamia na kuendeleza tasnia ya mazao ya bustani kutokana na mchango mkubwa wa tasnia hiyo kwenye mapato ya fedha za kigeni.

Mheshimiwa Spika, Wizara imeandaa mapendekezo ya kufanya marekebisho madogo Miscellaneous Amendment ya Sheria ya Usalama wa Chakula Na. 10 ya mwaka 1991 iliyoanzisha Mamlaka ya Udhibiti wa Nafaka na Mazao Mchanganyiko - Cereal and Other Produce Regulatory Authority, ambapo pamoja na mambo mengine majukumu ya Mamlaka hiyo yatarekebishwa ili kuipa jukumu mahsusi la usimamizi na uendelezaji wa tasnia ya bustani.