Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Dr. Florence George Samizi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Muhambwe

Primary Question

MHE. DKT. FLORENCE G. SAMIZI aliuliza: - Je, ni lini Serikali itajenga minara ya simu na TBC Redio katika Jimbo la Muhambwe?

Supplementary Question 1

MHE. DKT. FLORENCE G. SAMIZI: Mheshimiwa Spika, ahsante sana kwa kunipa nafasi ya kuuliza maswali madogo ya nyongeza.

Mheshimiwa Spika, kwanza kabisa ninaishukuru Serikali kwa kutuwekea mpango mzuri wa kutuletea minara katika Jimbo letu. Hata hivyo, Jimbo la Muhambwe lina mnara mmoja tu wa TTCL ambao umelemewa na badala yake inatumia kufanya roaming kwa minara ya kampuni nyingine.

Je, Serikali haioni sasa ni muda muafaka wa kuweka minara mingi ya TTCL ili tuweze kupata usikivu lakini pia mawasiliano ya bei nafuu?

(b) Mheshimiwa Spika, tunaishukuru Serikali pia kwa kutuletea kifaa hicho ambacho kitaenda kuboresha usikivu wa TBC Redio katika Jimbo letu, hata hivyo usikivu wa TBC Redio katika Jimbo letu ni hafifu sana inayopelekea wananchi wa Muhambwe kusikiliza zaidi Redio ya Burundi kuliko ya TBC Redio.

Je, nini mkakati wa Serikali kuboresha zaidi usikivu wa Radio katika Jimbo zima la Muhambwe? (Makofi)

Name

Kundo Andrea Mathew

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bariadi

Answer

NAIBU WAZIRI WA HABARI, MAWASILIANO NA TEKNOLOJIA YA HABARI: Mheshimiwa Spika, naomba kujibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Dkt. Florence George Samizi Mbunge wa Muhambwe kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, kwanza kabisa nimpongeze Mheshimiwa Mbunge kwa kazi nzuri ambayo anaifanya, hivi leo nimejulishwa na Mheshimiwa Waziri amekuwa akiwasiliana nae kukumbushia kuhusu zile ahadi zake katika kipindi cha kampeni, Mheshimiwa Waziri ameshatoa maelekezo na ahadi hizo ambazo zinalenga katika Wizara yetu zitafanyiwa kazi zote. Vilevile suala la usikivu kama ambavyo nimejibu katika swali la msingi ni kwamba kifaa hiki kitakaporejeshwa na kufanyiwa majaribio nina uhakika kabisa kwamba tatizo la usikivu katika Jimbo la Muhambwe litakuwa limemalizika kabisa. Ahsante. (Makofi)

Name

Mwantumu Mzamili Zodo

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. DKT. FLORENCE G. SAMIZI aliuliza: - Je, ni lini Serikali itajenga minara ya simu na TBC Redio katika Jimbo la Muhambwe?

Supplementary Question 2

MHE. MWANTUMU M. ZODO: Mheshimiwa Spika, ahsante sana changamoto za mawasiliano kwa Jimbo la Muhambwe zinafanana sana na changamoto za mawasiliano kwa Jimbo letu la Muheza katika Tarafa ya Amani ambayo ni Kata ya Amani Kisiwani Mbomole, Misalai, Zirai na Kwezitu: -

Je, ni lini sasa Serikali inakwenda kujenga minara ya simu ili kutatua changamoto ya mawasiliano kwa wananchi wa Tarafa ya Amani?

Name

Kundo Andrea Mathew

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bariadi

Answer

NAIBU WAZIRI WA HABARI, MAWASILIANO NA TEKNOLOJIA YA HABARI: Mheshimiwa Spika, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Mwantumu kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, Serikali inaendelea kuwekeza kuhakikisha kwamba inatatua changamoto ya mawasiliano kulingana na maelekezo ya Ilani ya Chama cha Mapinduzi. Jimbo la Muheza tumeliingiza katika mpango wa utekelezaji wa mradi wa Tanzania kidigitali, hivyo tunaamini kwamba kabla ya mwaka wa fedha huu haujaisha zabuni hii itakuwa imeshatangazwa na hatimaye mtoa huduma atapatikana kwa ajili ya Jimbo la Muheza. Ahsante sana. (Makofi)