Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 7 Sitting 11 Information, Culture, Arts and Sports Wizara ya Habari, Mawasiliano na Teknolojia ya Habari 94 2022-04-22

Name

Dr. Florence George Samizi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Muhambwe

Primary Question

MHE. DKT. FLORENCE G. SAMIZI aliuliza: -

Je, ni lini Serikali itajenga minara ya simu na TBC Redio katika Jimbo la Muhambwe?

Name

Kundo Andrea Mathew

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bariadi

Answer

NAIBU WAZIRI WA HABARI, MAWASILIANO NA TEKNOLOJIA YA HABARI alijibu: -

Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Habari, Mawasiliano na Teknolojia ya Habari naomba kujibu swali la Mheshimiwa Dkt. Florence George Samizi, Mbunge wa Muhambwe, lenye sehemu (a) na (b) kama ifuatavyo: -

(a) Kuhusu Ujenzi wa Minara ya simu, Serikali itajenga minara ya mawasiliano katika Kata za Bunyambo, Murungu na Nyaruyoba ambazo zimebainika kuwa na changamoto ya upatikanaji wa huduma za mawasiliano katika Jimbo la Muhambwe. Zabuni ya minara hiyo itatangazwa kabla ya mwaka wa fedha wa 2021/2022 kukamilika.

(b) Kuhusu TBC Redio, mtambo wa masafa ya FM katika Jimbo la Muhambwe, Mwezi Machi, 2022 mtambo huo ulipigwa na radi iliyoharibu vipuri vyake. Vipuri hivyo vimeshaagizwa na tayari vimeshawasili nchini. Kazi ya kufunga vipuri hivyo itakapokamilika, na kuwashwa na kufanyiwa majaribio ya kiufundi kabla ya tarehe 30 Mei 2022 hivyo kurejesha usikivu wa TBC katika Jimbo la Muhambwe na maeneo ya jirani. Ahsante. (Makofi)