Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Oran Manase Njeza

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mbeya Vijijini

Primary Question

MHE. ORAN M. NJEZA aliuliza: - Je, Serikali ina mkakati gani wa kupunguza bei za mbolea zinazopanda kwa kasi kwenye Soko la Dunia ili kumpunguzia mkulima mzigo?

Supplementary Question 1

MHE. ORAN M. NJEZA: Mheshimiwa Spika, nashukuru. Pamoja na majibu mazuri ya Serikali, ningependa kuuliza maswali mawili ya nyongeza. Kwa kuwa katika Wilaya ya Mbeya, kuna madini ya aina ya calcium carbonate kwa wingi na NDC katika miaka ya 2006/2007 walikuwa na mkakati wa kuanzisha kiwanda ili watengeneze mbolea, CAN: Je, ni lini Serikali itaanza kujenga kiwango hicho kwa kushirikiana na NDC?

Mheshimiwa Spika, swali la pili; kwa kuwa bei hizi za mbolea zinatishia upungufu mkubwa wa chakula: Je, Serikali ina mpango gani wa kuhakikisha inarudisha ruzuku kama ilivyo kwenye nchi nyingine za SADC na Afrika Mashariki?

Mheshimiwa Spika, nashukuru sana.

Name

Anthony Peter Mavunde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Dodoma mjini

Answer

NAIBU WAZIRI WA KILIMO: Mheshimiwa Spika, napenda kujibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Oran Manase Njeza, Mbunge wa Mbeya Vijijini, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, swali la kwanza la ujenzi wa kiwanda, ni dhamira ya Serikali kuona ujenzi wa viwanda vingi zaidi vya mbolea vinakuwepo hapa nchini ili kutatua changamoto ya upatikanaji wa mbolea na kupunguza bei ya mbolea na kupunguza bei ya mbolea kama ilivyo sasa. Nimwondoe hofu Mheshimiwa Mbunge kwamba sisi kama Wizara pamoja na wenzetu wa Wizara ya Viwanda, Biashara na Uwekezaji, tutakaa pamoja ili tuhakikishe kwamba wazo hili ambalo lilianzishwa mwaka 2006 liweze kukamilika na kuwapungizia adha wakulima.

Mheshimiwa Spika, la pili, ni la kuhusu ruzuku. Katika bajeti yetu ambayo tutaisoma mwezi ujao na pia katika utekelezaji ambao utaanza mwaka ujao wa fedha, tumedhamiria kutenga mfuko maalum (price stabilization fund) kwa ajili ya kudhibiti upandaji wa bei ya pembejeo ikiwemo na bei za mazao.

Mheshimiwa Spika, hivyo, nimwondoe hofu Mheshimiwa Mbunge kwamba hii ni sehemu ambayo pia tunaipa umuhimu mkubwa na Serikali imedhamiria kuanzisha mfuko wa ruzuku ambao utahakikisha unasaidia kupunguza maumivu ya wakulima na hasa katika upatikanaji wa bei ya mbolea ambayo itakuwa ni rafiki kwa mkulima.

Name

Issaay Zacharia Paulo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mbulu Mjini

Primary Question

MHE. ORAN M. NJEZA aliuliza: - Je, Serikali ina mkakati gani wa kupunguza bei za mbolea zinazopanda kwa kasi kwenye Soko la Dunia ili kumpunguzia mkulima mzigo?

Supplementary Question 2

MHE. ZACHARIA P. ISSAAY: Mheshimiwa Spika, nakushukuru. Pamoja na majibu mazuri ya Serikali na kwa kuwa viwanda vilivyotajwa ni viwili tu nchini: Je, Serikali haioni kuwa ni wakati muafaka sasa wa kuhamasisha wawekezaji wengine ili uzalishaji wa mbolea nchini uwe mkubwa?

Name

Anthony Peter Mavunde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Dodoma mjini

Answer

NAIBU WAZIRI WA KILIMO: Mheshimiwa Spika, napenda kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Zacharia Issaay, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, kama nilivyosema awali, moja kati ya mikakati tuliyonayo hivi sasa ni kuendelea kuwakaribisha wawekezaji wengi zaidi wa viwanda vya mbolea ili kwa pamoja tusaidiane kutatua changamoto iliyoko hivi sasa ya upatikanaji wa mbolea. Tunaamini katika misimu michache inayokuja, kiwanda cha Itracom na Minjingu ambacho sisi kama Wizara tumewasaidia kuzungumza na Benki za TADB na CRDB kuongeza expansion, tutakuwa tumetatua changamoto hii ya upatikanaji wa mbolea kwa kiwango kikubwa sana. Pia bado tunakaribisha makampuni mengine, na kama Serikali tunaendelea pia kukaribisha makampuni mengi zaidi ili tuondokane na changamoto hii ya upatikanaji wa mbolea hapa nchini.