Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 7 Sitting 11 Livestock , Fisheries, Agriculture, Food Security and Cooperatives Wizara ya Kilimo 90 2022-04-22

Name

Oran Manase Njeza

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mbeya Vijijini

Primary Question

MHE. ORAN M. NJEZA aliuliza: -

Je, Serikali ina mkakati gani wa kupunguza bei za mbolea zinazopanda kwa kasi kwenye Soko la Dunia ili kumpunguzia mkulima mzigo?

Name

Anthony Peter Mavunde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Dodoma mjini

Answer

NAIBU WAZIRI WA KILIMO alijibu: -

Mheshimiwa Spika, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Oran Manase Njeza, Mbunge wa Mbeya Vijijini, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, katika msimu wa 2021/2022 bei ya mbolea imeendelea kupanda katika Soko la Dunia kutokana na athari za UVIKO-19 na Vita ya Urusi na Ukraine zilizosababisha kupungua kwa uzalishaji na ongezeko la gharama za malighafi zinazotumika kutengeneza mbolea.

Mheshimiwa Spika, kutokana na hali hiyo, Serikali imeanza kuchukuliwa hatua za haraka, muda wa kati na muda mrefu katika kukabiliana na changamoto ya kupanda kwa bei. Hatua za haraka ni pamoja na kudhibiti upandaji holela wa bei usiozingatia gharama halisi za uingizaji mbolea nchini kwa kutangaza bei elekezi zinazopaswa kuzingatiwa na wafanyabiashara katika maeneo ya uzalishaji.

Mheshimiwa Spika, Serikali imekutana na uongozi wa kiwanda cha mbolea cha Minjingu kwa lengo la kuzipatia ufumbuzi changamoto za kiwanda ili kuhakikisha kinaongeza uzalishaji wa mbolea kutoka wastani wa tani 30,000 hadi kufikia tani 100,000 kwa mwaka. Aidha, Serikali inaendelea kuhamasisha wawekezaji wapya wa viwanda vya mbolea ambapo kampuni ya Intracom Fertilizers Limited kutoka Burundi imejitokeza na inajenga kiwanda katika Mkoa wa Dodoma chenye uwezo wa kuzalisha tani 600,000 kwa mwaka.

Mheshimiwa Spika, hatua hizo zinazochukuliwa na Serikali kwa kushirikiana na sekta binafsi zitasaidia kupunguza bei ya mbolea.