Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Boniphace Mwita Getere

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bunda

Primary Question

MHE. BONIPHACE M. GETERE K.n.y. MHE. JOSEPH K. MUSUKUMA aliuliza: - Je, ni lini Serikali itarudisha hekta elfu nane zilizopo kwenye Pori la Ruande Jimbo la Geita kwani pori hilo limepoteza sifa ya kuwa Hifadhi?

Supplementary Question 1

MHE. BONIPHACE M. GETERERE: Mheshimiwa Spika, nashukuru kwa majibu mazuri ya Serikali, nina swali moja tu la nyongeza. Kwa kuwa kumekuwepo na maeneo mengi hapa nchini yaliyokosa sifa ya kuwa hifadhi na yamekuwa na migogoro mikubwa sana na wananchi. Ni lini Serikali sasa itafanya tathmini ya maeneo yote haya na kuyaleta hapa ili tuyagawe kwa wananchi, yote yaliyokosa sifa? (Makofi)

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE): Mheshimiwa Spika, ahsante sana. Naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Boniphace Mwita Getere, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, ni kweli kwamba tumekuwa na maeneo mengi ambayo yamekuwa hifadhi kwa muda mrefu, lakini baadhi ya maeneo yamekuwa na changamoto ya migogoro kati ya wananchi pia na mamlaka za hifadhi.

Nimhakikishie kwamba Serikali inatambua changamoto katika maeneo hayo na tathmini inafanyika kwa kuzingatia sheria, taratibu na miongozo ya maeneo ya hifadhi ili kuhakikisha yale ambayo yanaendelea kukidhi sifa za kuwa maeneo ya hifadhi yaendelee kuwa maeneo ya hifadhi lakini yale ambayo yamepoteza sifa, Serikali inachukua hatua za kuendelea kuwapatia wananchi.

Mheshimiwa Spika, kwa hiyo nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba jambo hili tunalifanyia kazi ikiwemo la msitu huu ambao tumeujibia. Ahsante.

Name

Stanslaus Haroon Nyongo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Maswa Mashariki

Primary Question

MHE. BONIPHACE M. GETERE K.n.y. MHE. JOSEPH K. MUSUKUMA aliuliza: - Je, ni lini Serikali itarudisha hekta elfu nane zilizopo kwenye Pori la Ruande Jimbo la Geita kwani pori hilo limepoteza sifa ya kuwa Hifadhi?

Supplementary Question 2

MHE. STANSLAUS H. NYONGO: Mheshimiwa Spika, ahsante sana kwa kunipa nafasi. Napenda kumuuliza Mheshimiwa Naibu Waziri kwamba kwa mfano sisi pale katika Mkoa wa Simiyu tuna Pori la Maswa na ni pori kubwa na ni maarufu. Je, Serikali ina mkakati gani wa kutangaza mapori haya kimataifa ili yaweze kutumika kwa maana ya kukaribisha watalii, vilevile kuhakikisha kwamba wananchi wa maeneo haya wananeemeka na mapori haya?

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE): Mheshimiwa Spika, ahsante sana. Naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Stanslaus Nyongo, Mbunge wa Jimbo la Maswa Mashariki, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, ni kweli katika Halmashauri ya Maswa na Mkoa wa Simiyu kuna Pori maarufu la Maswa na kwamba Serikali imekuwa na mkakati wa kuhakikisha kwamba inatangaza mapori haya ili watalii waendelee kuja na Serikali yetu iendelee kupata mapato. Ndio maana hivi sasa tunaongea Mheshimiwa Rais wetu Mama Samia Suluhu Hassan anaendelea kuitangaza Royal Tour ili tuhakikishe watalii zaidi wanaendelea kuongezeka katika hifadhi zetu lakini maeneo ya kitalii ikiwepo Pori la Maswa. Kwa hiyo nimhakikishie kwamba mpango wa Serikali ni huo na utahakikisha kwamba wananchi wanaoishi maeneo ya jirani pia wananufaika na mpango huo, ahsante.