Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 7 Sitting 11 Regional Administration and Local Government Authorities Ofisi ya Rais TAMISEMI. 88 2022-04-22

Name

Joseph Kasheku Musukuma

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Geita

Primary Question

MHE. BONIPHACE M. GETERE K.n.y. MHE. JOSEPH K. MUSUKUMA aliuliza: -

Je, ni lini Serikali itarudisha hekta elfu nane zilizopo kwenye Pori la Ruande Jimbo la Geita kwani pori hilo limepoteza sifa ya kuwa Hifadhi?

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE) alijibu: -

Mheshimiwa Spika, ahsante sana. Kwa niaba ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, TAMISEMI, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Joseph Kasheku Musukuma, Mbunge wa Geita Vijijini, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, Msitu wa Hifadhi Ruande ulianzishwa kwa GN Na.106 ya mwaka 1956 una ukubwa wa Hekta 15,550. Msitu huu unaosimamiwa na Halmashauri ya Wilaya ya Geita umekuwa ukivamiwa kwa shughuli za kilimo na ufugaji unaofanywa na wananchi wa vijiji 13 vinavyouzunguka.

Mheshimiwa Spika, Serikali ilipokea maombi kutoka katika Vijiji viwili (2) vya Kagu na Kakubilo ya kumegewa sehemu ya hifadhi hiyo kwa shughuli za kilimo. Serikali inayafanyia tathmini maombi hayo kupitia Kamati ya Mawaziri Nane wa Kisekta inayoshughulikia migogoro ya vijiji 975 nchini kote na itatoa maamuzi muafaka kwa kuzingatia maslahi ya pande zote.