Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Ussi Salum Pondeza

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chumbuni

Primary Question

MHE. USSI SALUM PONDEZA aliuliza: - Je, ni lini Serikali itajenga majengo ya Wizara ya Elimu Zanzibar ili kutoa huduma kwa wakati na kupunguza gharama za kukodi Ofisi?

Supplementary Question 1

MHE. USSI SALUM PONDEZA: Mheshimiwa Spika, kwanza napenda kumpongeza Mheshimiwa Waziri kwa majibu yake mazuri, kwanza nilikuwa na maswali mawili ya nyongeza. Kutokana na mpango huu ambao majibu yake ya Serikali ambayo ameelezea nataka nimuulize Zanzibar inanufaikaje na mradi huu wa High Education Economic?

Mheshimiwa Spika, swali la pili, napenda kumwuliza, Serikali ina mpango gani sasa wa kuzipandisha hadhi campus za UDSM na Mwalimu Nyerere ili ziwe Chuo Kikuu ili kuondosha tatizo hili? Ahsante.

Name

Omary Juma Kipanga

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mafia

Answer

NAIBU WAZIRI WA ELIMU, SAYANSI NA TEKNOLOJIA: Mheshimiwa Spika, naomba kujibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Ussi Pondeza, Mbunge wa Chumbuni, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, ni kweli Serikali yetu ilipata mkopo, kutoka Benki ya Dunia wenye thamani ya zaidi ya Dola za Marekani milioni 425. Naomba nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge katika mkopo huu, Serikali imetenga zaidi ya Dola milioni 20 kwa ajili ya Chuo chetu cha Taifa cha Zanzibar, kwa ajili ya uongezaji wa miundombinu pamoja na usomeshaji wa wafanyakazi katika eneo lile. Kwa hiyo, eneo hili tunakwenda kulifanyia maboresho makubwa sana kuhakikisha kwamba tunakuwa na miundombinu ya kutosha; na Zanzibar ni mnufaika mkubwa wa mikopo hii pamoja na vyuo vingine vya elimu ya juu nchini.

Mheshimiwa Spika, katika swali lake la pili, ameulizia kuhusiana na suala la kupandisha hadhi campus zetu. Naomba nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge na Bunge lako Tukufu, hivi sasa Serikali kupitia mkopo huu wa HIT, tunakwenda kuboresha miundombinu katika vyuo vyetu vikuu na taasisi mbalimbali za elimu ya juu nchini.

Mheshimiwa Spika, kwa sasa hatuna dhamira ya kupandisha hadhi campus hizi mbili pamoja na campus nyingine za vyuo zilizokuweko pale mpaka miundombinu pamoja na watumishi waweze kutosheleza mahitaji tunayoyahitaji hivi sasa. Nashukuru sana. (Makofi)