Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 7 Sitting 10 Education, Science,Technology and Vocational Training, Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia 86 2022-04-21

Name

Ussi Salum Pondeza

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chumbuni

Primary Question

MHE. USSI SALUM PONDEZA aliuliza: -

Je, ni lini Serikali itajenga majengo ya Wizara ya Elimu Zanzibar ili kutoa huduma kwa wakati na kupunguza gharama za kukodi Ofisi?

Name

Omary Juma Kipanga

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mafia

Answer

NAIBU WAZIRI WA ELIMU, SAYANSI NA TEKNOLOJIA alijibu: -

Mheshimiwa Spika, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Ussi Salum Pondeza, Mbunge Chumbuni, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, Zanzibar kuna Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Amali, yenye majengo yake, ambayo ina Idara ya Elimu ya Juu inayoongozwa na Mkurugenzi kwa lengo la kuhakikisha kuwa wanafunzi wa elimu ya juu wanapata huduma. Vilevile, zipo Taasisi za Elimu ya Juu zinazotoa huduma kwa wanafunzi kama vile; Chuo Kikuu cha Taifa Zanzibar, Bodi ya Mikopo ya Elimu ya Juu, Chuo Kikuu Huria cha Tanzania, Taasisi ya Kumbukumbu ya Mwalimu Nyerere, Taasisi ya Sayansi na Teknolojia Karume, Taasisi ya Sayansi ya Bahari (IMS) na Tume ya Taifa Sayansi na Teknolojia (COSTECH).

Mheshimiwa Spika, Serikali imeendelea kujenga ofisi katika maeneo mbalimbali nchini kwa lengo la kusogeza huduma za elimu karibu na wananchi kulingana na upatikanaji wa fedha. Aidha, ni nia ya Serikali kuhakikisha kuwa kila Taasisi ya Umma inakuwa na majengo yake kwa lengo la kupunguza gharama za kukodi ofisi. Nakushukuru sana. (Makofi)