Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Antipas Zeno Mgungusi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Malinyi

Primary Question

MHE. ANTIPAS Z. MGUNGUSI aliuliza: - Je, ni lini Serikali itajenga walau kilometa chache barabara ya Lupiro – Malinyi – Kilosa kwa Mpepo – Londo mpaka Lumecha kilometa 296?

Supplementary Question 1

MHE. ANTIPAS Z. MGUNGUSI: Mheshimiwa Spika, nashukuru kwa majibu mazuri ya Serikali lakini barabara hiyo ambayo anaizungumzia kwa sasa kuna dharura kwa maana ya mawasiliano yamekatika baina ya Malinyi na Morogoro Mjini.

Je, Wizara iko tayari kuiongezea TANROADS Mkoa fedha na kuielekeza ku-attend dharura hii? (Makofi)

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE): Mheshimiwa Spika, ahsante. Naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Antipas Zeno Mgungusi Mbunge wa Malinyi kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, ni kweli barabara ya Malinyi ni kati ya wilaya ambazo ziko chini na hii barabara mvua nyingi zinazonyesha milimani zinapita huko, kwa hiyo kuna changamoto kubwa ya mvua kupita juu ya barabara. Kwa kulitambua hilo nataka nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge Serikali imeliona na mpango kwanza ni kuongeza fedha kwa maana ya bajeti ili tuweze kuinua hiyo barabara na kuongeza makalavati sehemu ambazo maji mengi yanapita. Ahsante.

Name

Cecil David Mwambe

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ndanda

Primary Question

MHE. ANTIPAS Z. MGUNGUSI aliuliza: - Je, ni lini Serikali itajenga walau kilometa chache barabara ya Lupiro – Malinyi – Kilosa kwa Mpepo – Londo mpaka Lumecha kilometa 296?

Supplementary Question 2

MHE. CECIL D. MWAMBE: Mheshimiwa Spika, nakushukuru sana kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali la nyongeza.

Barabara ya Lupio – Malinyi- Kilosa kwa Mpepo- Londo mpaka Lumecha ina umuhimu sana sawasawa na ilivyo barabara ya Masasi -Nachingwea - Liwale- Lupilo - Malinyi mpaka Kilosa inaunganisha Mkoa wa Lindi na Mtwara. Nini mkakati wa Serikali kuunganisha kipande hiki cha barabara ili kuwasaidia wakazi wa Mkoa wa Mtwara na Lindi kufika Dodoma kirahisi? (Makofi)

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE): Mheshimiwa Spika, ahsante. Naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Cecil Mwambe, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, barabara hii iko kwenye mpango wa Serikali kuijenga, kwa hiyo nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba kadri Serikali inavyopata fedha barabara hii itajengwa ili kurahisisha mawasiliano kati ya Wilaya hizo mbili. Ahsante.

Name

Dennis Lazaro Londo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mikumi

Primary Question

MHE. ANTIPAS Z. MGUNGUSI aliuliza: - Je, ni lini Serikali itajenga walau kilometa chache barabara ya Lupiro – Malinyi – Kilosa kwa Mpepo – Londo mpaka Lumecha kilometa 296?

Supplementary Question 3

MHE. DENNIS L. LONDO: Mheshimiwa Spika, nashukuru kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali la nyongeza.

Mheshimiwa Spika, barabara hii ya Londo -Lumecha ni muhimu sana lakini inayofanana na barabara ya Londo ni barabara ya kutoka Kilosa mpaka Ulaya kwenda Mikumi.

Je, ni lini Serikali inaenda kuanza ujenzi wa barabara hii? (Makofi)

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE): Mheshimiwa Spika, ahsante. Naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Dennis Londo, Mbunge wa Mikumi, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, barabara hii ilishaanza kujengwa na tuna mpango wa kuendeleza. Naomba nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba azma ya Serikali ni kuunganisha barabara inayounganisha barabara ya Dodoma – Morogoro kwenda Mikumi ili iweze kujengwa yote kwa kiwango cha lami. Kwa hiyo nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba mipango ipo na bado tutaendelea kuikamilisha hiyo barabara kwa kiwango cha lami. Ahsante.

Name

Mrisho Mashaka Gambo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Arusha Mjini

Primary Question

MHE. ANTIPAS Z. MGUNGUSI aliuliza: - Je, ni lini Serikali itajenga walau kilometa chache barabara ya Lupiro – Malinyi – Kilosa kwa Mpepo – Londo mpaka Lumecha kilometa 296?

Supplementary Question 4

MHE. MRISHO M. GAMBO: Mheshimiwa Spika, kwa sababu changamoto ya barabara kwenye Jimbo la Malinyi inafanana na changamoto ya barabara kwenye Jimbo la Arusha Mjini. Naomba kuuliza swali kwa Mheshimiwa Naibu Waziri. Je, Serikali ina mpango gani wa kujenga barabara kutoka kwenye airport ya Kisongo mpaka eneo la Kilombero kwa sababu barabara hiyo inasababisha mafuriko sana kwenye Kata ya Unga Limited, Osinyai na Sombetini?

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE): Mheshimiwa Spika, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Mrisho Gambo, Mbunge wa Arusha Mjini, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, Barabara ya kutoka Kisongo kwenda Kilombero ni barabara ambayo ipo kwenye mpango na tayari usanifu unaendelea ili kukamilisha na kuweza kuijenga kwa kiwango cha lami na kuondoa changamoto kwa wakazi wa Arusha ambayo wanaipata sasa hivi. Ahsante.

Name

Elibariki Emmanuel Kingu

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Singida Magharibi

Primary Question

MHE. ANTIPAS Z. MGUNGUSI aliuliza: - Je, ni lini Serikali itajenga walau kilometa chache barabara ya Lupiro – Malinyi – Kilosa kwa Mpepo – Londo mpaka Lumecha kilometa 296?

Supplementary Question 5

MHE. ELIBARIKI I. KINGU: Mheshimiwa Spika, nakushukuru sana. Naomba kujua ni lini Serikali itatekeleza ujenzi wa Barabara ya Singida- Sepuka-Ndago mpaka Kizaga yenye urefu wa kilomita 95 ambayo imeahidiwa kwenye Ilani zote za Uchaguzi 2015 -2020 na 2020 - 2025 lakini mpaka leo barabara hii haijaanza?

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE): Mheshimiwa Spika, napenda kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Kingu, Mbunge wa Singida, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, barabara aliyoianisha ni kweli imeainishwa kwenye Ilani ya Chama cha Mapinduzi na ni azma ya Serikali kuijenga hii barabara kwa kiwango cha lami kama ilivyoahidiwa. Nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba mipango ipo na katika utekelezaji wa Ilani wa miaka hii mitano nataka nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba barabara hii itajengwa kadiri fedha itakavyopatikana. Ahsante.

Name

Daniel Baran Sillo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Babati Vijijini

Primary Question

MHE. ANTIPAS Z. MGUNGUSI aliuliza: - Je, ni lini Serikali itajenga walau kilometa chache barabara ya Lupiro – Malinyi – Kilosa kwa Mpepo – Londo mpaka Lumecha kilometa 296?

Supplementary Question 6

MHE. DANIEL B. SILLO: Mheshimiwa Spika, ahsante; je, Serikali itaanza lini ujenzi wa Barabara ya Dareda - Bashnet mpaka Dongobesh kwa kiwango cha lami?

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE): Mheshimiwa Spika, napenda kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Sillo, Mbunge wa Babati Vijijini, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, ni kweli barabara hii iko kwenye mpango na naomba tu tusubiri bajeti kwamba barabara hii Dareda - Dongobesh Serikali ina mpango wa kuijenga kwa kiwango cha lami. Ahsante.

Name

Cecilia Daniel Paresso

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. ANTIPAS Z. MGUNGUSI aliuliza: - Je, ni lini Serikali itajenga walau kilometa chache barabara ya Lupiro – Malinyi – Kilosa kwa Mpepo – Londo mpaka Lumecha kilometa 296?

Supplementary Question 7

MHE. CECILIA D. PARESSO: Mheshimiwa Spika, nakushukuru kwa kunipa nafasi ili niweze kuuliza swali dogo la nyongeza. Kumekuwa na ahadi ya muda mrefu sana ya ujenzi wa kiwango cha lami barabara ya kutoka njia panda Oldiani-Mangola mpaka Matala Lalago ambayo inaunganisha Mkoa wa Arusha na Mkoa wa Simiyu.

Je, ni lini Serikali angalau hata kwa vipande itaanza kujenga barabara hii kwa kiwango cha lami?

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE): Mheshimiwa Spika, ahsante. Napenda kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Cecilia Paresso, Mbunge wa Viti Maalum, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, barabara hii itaanza kujengwa kwa vipande, lakini barabara itakayoanza kujengwa ni ya Babati kuja Mbulu - Hydom kwenda Sibiti kwa kiwango cha lami na tutaanza sehemu ya Mbulu kuja Hydom na hiyo aliyoitaja tutaanza baada ya muda kwa sababu ni barabara ambayo zinaenda parallel. Kwa hiyo tumeamua tuanze kwanza hii ya Babati – Mbulu - Hydom kwenda Sibiti halafu barabara aliyoitaja itafuata. Ahsante.

Name

Daniel Awack Tlemai

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Karatu

Primary Question

MHE. ANTIPAS Z. MGUNGUSI aliuliza: - Je, ni lini Serikali itajenga walau kilometa chache barabara ya Lupiro – Malinyi – Kilosa kwa Mpepo – Londo mpaka Lumecha kilometa 296?

Supplementary Question 8

MHE. DANIEL A. TLEMAI: Mheshimiwa Spika, ahsante kwa kunipa nafasi. Barabara aliyoitaja ya Mbulu- Singida ni tofauti na barabara ambayo ameuliza muuliza swali ambayo inatoka njia panda ambayo inaelekea Mangola ambayo inaelekea Matala ambayo inaelekea Lalago ambayo pia imeunganisha Mkoa wa Arusha na Mkoa wa Simiyu. Sasa ni lini Serikali itatoa majibu sahihi ya barabara hiyo kuanza kama alivyotoa majibu ya barabara ya Mbulu-Singida?

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE): Mheshimiwa Spika, ahsante. Napenda kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Awack, Mbunge wa Babati, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, ziko barabara mbili ambazo nazifahamu kutokea Babati. Aliyoitaja Mheshimiwa Mbunge na niliyoitaja ni barabara ambazo zinakwenda parallel na zinakwenda kukutana mbele. Nimesema Serikali imeamua kujenga kwanza Barabara ya Serengeti bypass ambayo inaanzia Babati – Mbulu - Haydom kwenda Sibiti. Ahsante.

Name

Dr. Christine Gabriel Ishengoma

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. ANTIPAS Z. MGUNGUSI aliuliza: - Je, ni lini Serikali itajenga walau kilometa chache barabara ya Lupiro – Malinyi – Kilosa kwa Mpepo – Londo mpaka Lumecha kilometa 296?

Supplementary Question 9

MHE. DKT. CHRISTINE G. ISHENGOMA: Mheshimiwa Spika, ahsante sana kwa kunipatia nafasi ya kuuliza swali dogo la nyongeza. Je, ni lini Serikali itaanza ujenzi wa barabara ya kuanzia Ifakara -Kihansi- Madeke mpaka Njombe? (Makofi)

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE): Mheshimiwa Spika, ahsante. Napenda kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Dkt. Christine Ishengoma, Mbunge wa Viti Maalum Morogoro, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, barabara aliyoitaja Serikali itaanza kujenga kadiri fedha itakapopatikana. Ahsante.

Name

Shabani Omari Shekilindi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Lushoto

Primary Question

MHE. ANTIPAS Z. MGUNGUSI aliuliza: - Je, ni lini Serikali itajenga walau kilometa chache barabara ya Lupiro – Malinyi – Kilosa kwa Mpepo – Londo mpaka Lumecha kilometa 296?

Supplementary Question 10

MHE. SHABAN O. SHEKILINDI: Mheshimiwa Spika, ahsante sana kwa kuniona. Kwanza nishukuru Serikali kwa kututengea fedha za nusu kilomita kwa Barabara ya Magamba kwenda Mlalo na Barabara ya kutoka Magamba kwenda Mlola. Hata hivyo, mara nyingi tumekuwa tukiomba kwamba tuongezewe kilometa tano, je, Serikali ina mpango gani wa kuongeza kilometa tano ambazo tumeziomba? (Makofi)

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE): Mheshimiwa Spika, ahsante, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Shekilindi, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, ni kweli barabara hii tumeamua kuijenga kwa awamu na naomba nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kupitia Ofisi ya Meneja wa TANROAD wa Mkoa wa Tanga, barabara hii tutaenda kuijenga kwa awamu kadiri fedha zitakapopatikana. Kwa hiyo tutaendelea kuijenga kwa vipande vipande mpaka tukamilishe hizo kilomita tano. Ahsante.

Name

Vita Rashid Kawawa

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Namtumbo

Primary Question

MHE. ANTIPAS Z. MGUNGUSI aliuliza: - Je, ni lini Serikali itajenga walau kilometa chache barabara ya Lupiro – Malinyi – Kilosa kwa Mpepo – Londo mpaka Lumecha kilometa 296?

Supplementary Question 11

MHE. VITA R. KAWAWA: Mheshimiwa Spika, ahsante sana kwa kunipa fursa hii. Mheshimiwa Naibu Waziri alikuja kuitembelea Barabara yetu ya Mtwara Pachani - Nalasi na tulitoa ushauri kwamba kuna sehemu ya vipande vipande ambavyo ndivyo korofi vinasababisha watu kulala njiani. Je, Serikali ushauri wetu wa kututengenezea vile vipande korofi wameweka utaratibu gani ambavyo havizidi hata kilomita 10, vipande vile korofi korofi?

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE): Mheshimiwa Spika, ahsante. Napenda kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Vita Kawawa, Mbunge wa Namtumbo, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, ni kweli barabara hii nimeitembelea, barabara ambayo ndio inapita kwa wananchi. Mpango wa Serikali kama walivyoshauri Waheshimiwa Wabunge wa Jimbo hasa la Namtumbo na Tunduru tumewaagiza Meneja wa Mkoa wa Ruvuma waweze kuainisha maeneo yote korofi na madaraja korofi ili tuweze kuyatengeneza na kuondoa changamoto ya barabara hii kukatika kupitika kwa mwaka mzima.

Name

Eng. Stella Martin Manyanya

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Nyasa

Primary Question

MHE. ANTIPAS Z. MGUNGUSI aliuliza: - Je, ni lini Serikali itajenga walau kilometa chache barabara ya Lupiro – Malinyi – Kilosa kwa Mpepo – Londo mpaka Lumecha kilometa 296?

Supplementary Question 12

MHE. ENG. STELLA M. MANYANYA: Mheshimiwa Spika, ahsante. Je, ni lini Barabara kutoka Kitai-Rwanda-Litui mpaka Ndumbi itaanza kujengwa kwa kiwango cha lami?

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE): Mheshimiwa Spika, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Engineer Stella Manyanya, Mbunge wa Nyasa, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, barabara hii tayari iko kwenye hatua za awali na nataka nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba sasa hivi tunakamilisha usanifu wa kina na baada ya kukamilika usanifu wa kina kwa barabara hii ya kutoka Litui kwenda hadi Ndumbi na mpaka Nyasa tutaanza kuijenga kwa kiwango cha lami. Ahsante.