Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 7 Sitting 10 Works, Transport and Communication Wizara ya Ujenzi na Uchukuzi 83 2022-04-21

Name

Antipas Zeno Mgungusi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Malinyi

Primary Question

MHE. ANTIPAS Z. MGUNGUSI aliuliza: -

Je, ni lini Serikali itajenga walau kilometa chache barabara ya Lupiro – Malinyi – Kilosa kwa Mpepo – Londo mpaka Lumecha kilometa 296?

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE) alijibu: -

Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Ujenzi na Uchukuzi naomba kujibu swali la Mheshimiwa Antipas Zeno Mgungusi Mbunge wa Malinyi, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, Serikali imepokea ushauri wa Mheshimiwa Mbunge na itaanza kujenga kilometa chache chache za barabara ya Lupiro – Malinyi – Kilosa kwa Mpepo hadi Londo mpaka Lumecha yenye urefu wa kilometa 296 hasa kwa kuanza na maeneo korofi ili barabara hii iweze kupitika kwa urahisi wakati wote wa mwaka. Aidha, Serikali itaendelea kutafuta fedha kwa ajili ya kuanza ujenzi wa barabara hii kwa kiwango cha lami.