Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Juliana Daniel Shonza

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. JULIANA D. SHONZA aliuliza: - Je, Serikali ina mpango gani wa kupeleka Watumishi wa Afya wa kutosha katika Kituo cha Afya cha Itaka?

Supplementary Question 1

MHE. JULIANA D. SHONZA: Mheshimiwa Spika, nashukuru.

Kwanza nianze kwa kuishukuru Serikali kwa sababu imetupatia fedha zaidi ya Shilingi Milioni 300 kwa ajili ya ujenzi wa wodi za upasuaji pamoja na wodi za akina mama katika kituo cha afya cha Itaka.

Je, Serikali sasa inatuhakikishieje kwamba ujenzi huu utakapokamilika watatupatia Daktari wa upasuaji ikizingatiwa kwamba mpaka sasa hatuna Daktari wa upasuaji lakini kituo kile cha afya cha Itaga kinahudumia Kata takribani Tano kwa maana ya Kata ya Harungu pamoja na Nambizo. Kwa hiyo nilitaka kufahamu commitment ya Serikali kwamba itatuletea lini Daktari wa upasuaji?

Mheshimiwa Spika, swali la pili mamlaka ya Mji mdogo wa Mlowo una wakazi takribani 100,000 lakini katika hali ya kusikitisha mpaka sasa hivi hatuna Kituo cha Afya pale na sasa hivi ninavyoongea tayari wananchi wamefyatua tofali zaidi ya 150,000 vilevile mamlaka ya Mji imetoa eneo heka kumiā€¦

SPIKA: Mheshimiwa Juliana Shonza uliza swali.

MHE. JULIANA D. SHONZA: Mheshimiwa Spika, naomba kufahamu sasa ni lini Serikali itatuletea fedha kwa ajili ya ujenzi wa Kituo cha Afya cha Mlowo?

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE): Mheshimiwa Spika, ahsante sana. Naomba kujibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Juliana Daniel Sh onza, Mbunge wa Viti Maalum, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, kwanza nianze kwa kumpongeza sana Mheshimiwa Shonza kwa namna ambavyo anawasemea wananchi wa Mkoa wa Songwe pia kwa namna ambavyo anaendelea kuwapa ushirikiano Waheshimiwa Wabunge wa Mkoa wa Songwe akiwepo Mheshimiwa Mwenisongole Mbunge wa Jimbo la Mbozi.

Mheshimiwa Spika, Serikali imepeleka fedha kwa ajili ya ujenzi wa jengo la upasuaji katika Kituo cha Afya cha Itaka na nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge baada ya jengo lile kukamilika tutapeleka Daktari ambaye atatoa huduma za upasuaji. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, pili kuhusiana na Kata ya Mlowo kuwa na wananchi wengi na haina kituo cha afya nina imani kwamba Mheshimiwa Mbunge wa Jimbo aliwasilisha vipaumbele vya Kata Tatu za kimkakati nasi tutakwenda kufanya tathmini na kuona kama Mlowo iko katika orodha hiyo basi tutatafuta fedha ili tuweze kujenga kituo cha afya. Ahsante. (Makofi)

Name

Minza Simon Mjika

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. JULIANA D. SHONZA aliuliza: - Je, Serikali ina mpango gani wa kupeleka Watumishi wa Afya wa kutosha katika Kituo cha Afya cha Itaka?

Supplementary Question 2

MHE. MINZA S. MJIKA: Mheshimiwa Spika, ahsante, napenda kuuliza swali.

Mheshimiwa Spika, katika Mkoa wa Simiyu tuna Wilaya Tatu ambazo zina upungufu wa watumishi wa afya. Wilaya ya Meatu, Bariadi na Maswa.

Je, ni lini Serikali itapeleka watumishi wa kutosha?

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE): Mheshimiwa Spika, ahsante sana. Naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Minza, Mbunge wa Viti Maalum, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, ni kweli katika Halmashauri hizi za Mkoa wa Simiyu kuna upungufu wa watumishi kama ilivyo kwenye Halmashauri nyingine zote hapa nchini, mpango wa Serikali ni kuendelea kuajiri watumishi kwa awamu na ndiyo maana ajira 7,612 zimetangazwa na Halmashauri hizi pia zitapewa kipaumbele katika kuwapelekea watumishi hao. (Makofi)

Name

Japhet Ngailonga Hasunga (CPA)

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Vwawa

Primary Question

MHE. JULIANA D. SHONZA aliuliza: - Je, Serikali ina mpango gani wa kupeleka Watumishi wa Afya wa kutosha katika Kituo cha Afya cha Itaka?

Supplementary Question 3

MHE. JAPHET N. HASUNGA: Mheshimiwa Spika, ahsante.

Mheshimiwa Spika, naomba kumuuliza Mheshimiwa Waziri katika Kata ya Nanyara pale Songwe pana kituo cha afya ambacho kimejengwa takribani zaidi ya miaka minne sasa na hakina wafanyakazi kabisa wa kutosha.

Je, Serikali ina mkakati gani wa kuhakikisha kwamba inapeleka wafanyakazi katika kituo hicho cha afya?

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE): Mheshimiwa Spika, nashukuru sana. Naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Japhet Hasunga Mbunge wa Vwawa kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, katika kituo hiki cha Nanyara ambacho kimekamilika zaidi ya miaka Minne iliyopita kina watumishi wachache, nimhakikishie kwamba mpango ni kuhakikisha tunapeleka watumishi ambao angalau watakidhi mahitaji ya kituo cha afya na hivyo tutahakikisha tunapeleka watumishi katika kituo hiki ili waweze kutoa huduma bora za afya. Ahsante. (Makofi)

Name

Deus Clement Sangu

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kwela

Primary Question

MHE. JULIANA D. SHONZA aliuliza: - Je, Serikali ina mpango gani wa kupeleka Watumishi wa Afya wa kutosha katika Kituo cha Afya cha Itaka?

Supplementary Question 4

MHE. DEUS C. SANGU: Mheshimiwa Spika, nakushukuru sana kwa nafasi hii.

Katika Halmashauri ya Wilaya ya Sumbawanga mpaka sasa tuna uhaba wa watumishi wa kada ya afya 660. Je, Serikali ina mpango gani wa kuleta watumishi katika kada hii ya afya?

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE): Mheshimiwa Spika, ahsante sana. Naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Deus Sangu kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, kipaumbele cha Serikali kwenye vituo vyote vya afya vilivyokamilika vinavyotoa huduma na ambavyo vinatarajiwa kuanza kutoa huduma ni kupeleka watumishi ili viweze kutoa huduma. Ndiyo maana kuna ajira ambazo zimetangazwa. Kwa hiyo nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge mkakati wa Serikali ni kuhakikisha watumishi wanakwenda kwenye kituo hicho pia na tutahakikisha watumishi wanakwenda kutoa huduma za afya pale. Ahsante. (Makofi)

Name

Dr. Christina Christopher Mnzava

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. JULIANA D. SHONZA aliuliza: - Je, Serikali ina mpango gani wa kupeleka Watumishi wa Afya wa kutosha katika Kituo cha Afya cha Itaka?

Supplementary Question 5

MHE. DKT. CHRISTINA C. MNZAVA: Mheshimiwa Spika, ahsante kunipa nafasi ya kuuliza swali la nyongeza.

Je, ni lini Serikali itapeleka watumishi wa kutosha katika Wilaya ya Kishapu, vituo vya afya vya Mwahalanga, Dulisi na Kishapu?

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE): Mheshimiwa Spika, ahsante sana. Naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Dkt. Christina Mnzava Mbunge wa Viti Maalum kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, kama nilivyojibu katika majibu yangu ya awali kwamba mkakati wa Serikali ni kuendelea kuajiri, vituo hivi vya afya ambavyo vina upungufu wa watumishi vitapelekewa watumishi kwenye ajira hii pia kwenye ajira zinazofuata. Ahsante. (Makofi)

Name

Dr. John Danielson Pallangyo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Arumeru-Mashariki

Primary Question

MHE. JULIANA D. SHONZA aliuliza: - Je, Serikali ina mpango gani wa kupeleka Watumishi wa Afya wa kutosha katika Kituo cha Afya cha Itaka?

Supplementary Question 6

MHE. DKT. JOHN D. PALLANGYO: Mheshimiwa Spika, nakushukuru sana na mimi kunipa nafasi niulize swali la nyongeza nalo liko hivi.

Mheshimiwa Spika, baada ya wafadhili waliokuwa wanaendesha kituo cha afya Momela kujiondoa watumishi pia ambao walikuwa wanalipwa na wale wafadhili Afrika waliondoka. Sasa hivi huduma zimedorora; Je, Serikali ina mpango gani wa kupeleka watumishi na wataalam kwa ajili ya kufanya huduma zikae vizuri? (Makofi)

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE): Mheshimiwa Spika, ahsante sana. Naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Dokta Pallangyo, Mbunge wa Arumeru Mashariki, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, tunatambua kwamba kuna upungufu wa watumishi katika kituo hicho cha afya na nimhakikishie kwamba tutaendelea kupeleka watumishi pale ili waendelee kutoa huduma za afya na tutaangalia katika ajira hizi na zinazofuata ili tuhakikishe kwamba kituo kile kinatoa huduma bora kwa wananchi.

Name

Anatropia Lwehikila Theonest

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. JULIANA D. SHONZA aliuliza: - Je, Serikali ina mpango gani wa kupeleka Watumishi wa Afya wa kutosha katika Kituo cha Afya cha Itaka?

Supplementary Question 7

MHE. ANATROPIA L. THEONEST: Mheshimiwa Spika, nakushukuru. Halmashauri ya Kyerwa ina vituo vya afya Vitatu licha ya kuwa na wakazi zaidi ya 600,000. Napenda kujua tayari kituo cha afya cha Kamuli kimekamilika changamoto imekuwa vifaatiba na Madaktari.

Ni lini madaktari watapelekwa ili hicho kituo kiweze kuongezeka na kusaidia kupunguza adha kwa wananchi?

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE): Mheshimiwa Spika, ahsante sana. Naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Anatropia Theonest Mbunge wa Viti Maalum kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, vituo vyote ambavyo vimekamilika na ndio maana jana wakati tunapitisha bajeti hapa tunashukuru Waheshimiwa Wabunge kwa kupitisha bajeti ya Wizara hii ya Ofisi ya Rais, TAMISEMI ambayo kwa kiasi kikubwa kwenye sekta ya afya tumeweka ununuzi wa vifaatiba pia na ajira za watumishi.

Mheshimiwa Spika, nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba katika kituo hiki cha afya katika Halmashauri ya Kyerwa pia tutahakikisha kinapata vifaatiba na watumishi ili kianze kutoa huduma bora zaidi za afya kwa wananchi. (Makofi)

Name

Agnes Elias Hokororo

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. JULIANA D. SHONZA aliuliza: - Je, Serikali ina mpango gani wa kupeleka Watumishi wa Afya wa kutosha katika Kituo cha Afya cha Itaka?

Supplementary Question 8

MHE. AGNES E. HOKORORO: Mheshimiwa Spika, ahsante. Serikali ina mpango gani wa kupeleka watumishi katika kituo cha afya Lukuledi ambacho kinakamilika ambacho kitahudumia Kata zaidi ya Tano?

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE): Mheshimiwa Spika, ahsante sana. Naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Agnes Hokororo Mbunge wa Viti Maalum, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, kituo cha afya hiki cha Lukuledi ambacho amekitaja Mheshimiwa Mbunge ni miongoni mwa vituo ambavyo vitapelekewa watumishi ili viendelee kutoa huduma bora za afya. Kwa hiyo, nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba tutakipa kipaumbele kituo cha afya hiki?

Name

Yahaya Omary Massare

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Manyoni Magharibi

Primary Question

MHE. JULIANA D. SHONZA aliuliza: - Je, Serikali ina mpango gani wa kupeleka Watumishi wa Afya wa kutosha katika Kituo cha Afya cha Itaka?

Supplementary Question 9

MHE. YAHAYA O. MASSARE: Mheshimiwa Spika, ahsante sana.

Kipo Kituo cha afya Rungwa ambacho tunaendelea na ujenzi na hakijasajiliwa kama kituo cha afya na watumishi ni wa zahanati. Je, sasa Serikali iko tayari kupeleka watumishi kwa Kituo hiki cha Afya cha Rungwa?

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE): Mheshimiwa Spika, ahsante sana. Naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Yahaya Massare, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, kituo hiki cha afya ambacho kinaendelea na ujenzi baada ya kukamilika tutafanya mpango wa kuhakikisha kwamba tunapeleka watumishi ili kianze kutoa huduma za afya. Ahsante. (Makofi)