Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Jackson Gedion Kiswaga

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kalenga

Primary Question

MHE. JACKSON G. KISWAGA aliuliza: - Je, ni lini Serikali itapeleka transfoma yenye uwezo mkubwa wa njia tatu katika Kijiji cha Nyamihuu Kata ya Nzihi Jimboni Kalenga?

Supplementary Question 1

MHE. JACKSON G. KISWAGA: Mheshimiwa Spika, nakushukuru sana. Ahsante kwa majibu mazuri. Pamoja na hayo nitakuwa na maswali mawili ya nyongeza. Lakini pia nitumie fursa hii pia kumshukuru Waziri wa Nishati, kulikuwa na mradi uliosimama wa Solar pale katika kijiji cha Kilambo na sasa amenihakikishia unatekelezwa na naona unaendelea. Namshukuru kwa hiyo hatua maana nchi itapata umeme lakini pia wananchi wangu watapata ajira.

Mheshimiwa Spika, Serikali ilitoa tamko kwamba ifikapo 2022 Disemba tutakuwa tumemaliza changamoto za umeme kwenye vijiji. Katika Jimbo la Kalenga tuna vijiji vitatu ambavyo havina umeme vya Lwato, Makombe pamoja na Chamgo. Ni nini tamko la Serikali kutimiza hii ahadi yake?

Mheshimiwa Spika, swali la pili Serikali ilitamka kwamba itapeleka umeme kwenye vitongoji kwa maana ya umeme jazilizi, lakini tuna vitongoji vingi ambavyo vimekuwa na malalamiko kwa mfano kanisani pale Kiwele, Banawano pale Tosamaganga pamoja na pale Mangalali.

Je, ni lini Serikali itakamilisha suala hili? Ahsante sana. (Makofi)

Name

Stephen Lujwahuka Byabato

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bukoba Mjini

Answer

NAIBU WAZIRI WA NISHATI: Mheshimiwa Spika, naomba kujibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Kiswaga, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, ni kweli Serikali iliahidi kwamba itakamilisha umeme katika vijiji vyote ambavyo havikuwa na umeme kufikia Disemba, 2022 na ahadi hiyo bado ipo kwa sababu mikataba ilishasainiwa na wakandarasi wako site katika hatua mbalimbali za utekelezaji wa mradi huu wa REA wa 300 mzunguko wa pili na tunaamini kwa kuendelea kusimamia mikataba hii kwa wakati itakamilika ili vijiji vyote ambavyo vilikuwa havina umeme viweze kupata umeme.

Mheshimiwa Spika, katika eneo la pili ni kweli kwamba tunavyo vitongoji vingi ambavyo bado havijafikiwa na huduma ya umeme, lakini Serikali kama ilivyoeleza kwenye swali la msingi ni kwamba tayari umeme jazilizi utaanza kutekelezwa katika mwaka wa fedha ujao na kwa kadri ya pesa inavyopatikana huduma hii itazidi kuendelezwa kuhakikisha kwamba vitongoji vyote vinapata umeme na watumiaji wote wanaweza kupata umeme kwa wakati.

Name

Emmanuel Peter Cherehani

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ushetu

Primary Question

MHE. JACKSON G. KISWAGA aliuliza: - Je, ni lini Serikali itapeleka transfoma yenye uwezo mkubwa wa njia tatu katika Kijiji cha Nyamihuu Kata ya Nzihi Jimboni Kalenga?

Supplementary Question 2

MHE. EMMANUEL P. CHEREHANI: Mheshimiwa Spika, ahsante. Nikushukuru sana.

Mheshimiwa Spika, Jimbo la Ushetu lina changamoto kubwa sana ya umeme, hasa maeneo ya vijijini, maeneo ya shuleni, hospitalini na hata maeneo ambapo umeme upo unakatika katika sana.

Je, ni lini Serikali itapeleka umeme wa uhakika kwa wananchi wa Jimbo la Ushetu? (Makofi)

Name

Stephen Lujwahuka Byabato

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bukoba Mjini

Answer

NAIBU WAZIRI WA NISHATI: Mheshimiwa Spika, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Cherehani kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, katika bajeti ya Mwaka wa Fedha 2022/2023 Serikali imetenga takribani Shilingi Bilioni 400 ili kuboresha na kuimarisha gridi yetu ya Taifa na hivyo tunaamini baada ya kupata hizo pesa na mradi wa kuboresha gridi ya Taifa kutekelezwa, tatizo la kukatika katika kwa umeme litaendelea kupungua kwa sehemu kubwa.

Mheshimiwa Spika, pia katika eneo hilo umeme vijijini bado unaendelea kupelekwa kwa mikataba ambayo ipo na eneo la Shinyanga kwenye Jimbo lake ni eneo ambalo tayari lina Mkandarasi na anaendelea na kazi.

Name

Edwin Enosy Swalle

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Lupembe

Primary Question

MHE. JACKSON G. KISWAGA aliuliza: - Je, ni lini Serikali itapeleka transfoma yenye uwezo mkubwa wa njia tatu katika Kijiji cha Nyamihuu Kata ya Nzihi Jimboni Kalenga?

Supplementary Question 3

MHE. EDWIN E. SWALLE: Mheshimiwa Spika, ahsante sana kunipa nafasi. Maeneo mengi nchini wananchi wamehamasika kuomba umeme kwenye vitongoji vyao na vijiji. Katika Jimbo la Lupembe wananchi wangu wa Upami, Iyembela na maeneo mengine wamejaza fomu za kulipia umeme lakini kwa muda mrefu hawapewi.

Je, ni nini maelekezo ya Serikali inapotokea wananchi wamelipia umeme lakini hawaingiziwi kwenye maeneo yao?

Name

Stephen Lujwahuka Byabato

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bukoba Mjini

Answer

NAIBU WAZIRI WA NISHATI: Mheshimiwa Spika, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Swalle wa Jimbo la Lupembe kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, ni kweli kwamba kuna kipindi ambapo mahitaji ya umeme yalikuwa makubwa sana kwa sababu ya mazingira tuliyokuwa nayo kuliko uwezo wa TANESCO wa kuunganisha kwa wakati. Tunaendelea kujipanga na Serikali imeelekeza inapoanza Julai hatutarajii na hatutakiwi kuwa na kiporo cha zaidi ya mwezi mmoja nyuma, ndiyo mpango wa Serikali na imeongeza bajeti katika maeneo ya uunganishaji ili kuhakikisha kwamba basi mtu anapoomba umeme angalau ndani ya mwezi mmoja awe ameupata kuhakikisha kwamba anaweza kuutumia kwa wakati kwa mahitaji yake. (Makofi)

Name

Oliver Daniel Semuguruka

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. JACKSON G. KISWAGA aliuliza: - Je, ni lini Serikali itapeleka transfoma yenye uwezo mkubwa wa njia tatu katika Kijiji cha Nyamihuu Kata ya Nzihi Jimboni Kalenga?

Supplementary Question 4

MHE. OLIVER D. SEMUGURUKA: Mheshimiwa Spika, nakushukuru sana kwa kuniona.

Mradi wa umeme wa Rusumo uliopo Wilaya ya Ngara ulitarajia kukamilika Desemba mwaka jana 2021 lakini mradi huo mpaka sasa haujakamilika.

Je, ni lini Serikali itakamilisha mradi huo ili kutatua tatizo la umeme Wilaya ya Ngara na Kagera kwa ujumla? (Makofi)

Name

Stephen Lujwahuka Byabato

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bukoba Mjini

Answer

NAIBU WAZIRI WA NISHATI: Mheshimiwa Spika, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Oliver Semuguruka, Mbunge wa Viti Maalum kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, ni kweli mradi wa umeme wa Rusumo unaotarajiwa kuzalisha megawatts 87 unatekelezwa na ubia wa nchi tatu ambazo ni Tanzania, Ruanda na Burundi. Ni kweli ulitarajiwa ukamilike Desemba mwaka jana lakini kwa sababu ya changamoto za ugonjwa wa UVIKO-19 ambao wenzetu uliwakabili zaidi yetu, mradi huo umechelewa lakini maelekezo ya Serikali hizi tatu ni kwamba ifikapo Novemba mwaka huu mradi huu uweze kukamilika ili wale wananchi ambao Mheshimiwa Oliver anawafuatilia wa Jimbo la Ngara lakini na wa Mkoa wa Kagera kwa ujumla na Tanzania kwa ujumla waweze kunufaika na upatikanaji wa umeme unaotoka kwenye mradi huu wa Rusumo. (Makofi)

Name

Conchesta Leonce Rwamlaza

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. JACKSON G. KISWAGA aliuliza: - Je, ni lini Serikali itapeleka transfoma yenye uwezo mkubwa wa njia tatu katika Kijiji cha Nyamihuu Kata ya Nzihi Jimboni Kalenga?

Supplementary Question 5

MHE. CONCHESTA L. RWAMLAZA: Mheshimiwa Spika, ahsante sana kwa kunipa nafasi.

Mheshimiwa Spika, transformer zinapoharibika na hasa vijijini huchukua muda mrefu bila kurejeshwa au kufanyiwa matengenezo na wakati mwingine inapita hata miezi sita.

Je, Serikali ina mpango gani wa kuhakikisha kwamba hizi transforme zinapoharibika zinarejeshwa kwa wakati ambao haumizi wananchi? (Makofi)

Name

Stephen Lujwahuka Byabato

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bukoba Mjini

Answer

NAIBU WAZIRI WA NISHATI: Mheshimiwa Spika, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Conchesta Rwamlaza kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, ni kweli siku za nyuma manunuzi yalikuwa yanafanyika centrally na hivyo procedure zilikuwa zinachelewa kutoka kwenye Wilaya, Mikoa, Kanda mpaka kuja Taifa lakini kwa sasa TANESCO imeboresha utaratibu wake na kushusha manunuzi haya kwenye ngazi za Kanda mpaka kwenye ngazi za Mikoa na hivyo kurahisisha manunuzi kwa wakati.

Mheshimiwa Spika, kwenye bajeti inayokuja ambayo tutakuja kuiwasilisha hapa imetengwa fungu la ziada la kufanya matengenezo kwenye maeneo haya, kwa hiyo pesa itapatikana kwa haraka na kuweza kurekibisha maeneo ambayo yatakuwa yanapata matatizo ili kuwapa huduma wananchi.

Name

Sylivia Francis Sigula

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. JACKSON G. KISWAGA aliuliza: - Je, ni lini Serikali itapeleka transfoma yenye uwezo mkubwa wa njia tatu katika Kijiji cha Nyamihuu Kata ya Nzihi Jimboni Kalenga?

Supplementary Question 6

MHE. SYLVIA F. SIGULA: Mheshimiwa Spika, ahsante kwa kunipa nafasi.

Mheshimiwa Spika, kumekuwa na tatizo sugu la kukatika katika kwa umeme Mkoani Kigoma hasa katika Wilaya ya Kigoma Mjini na Kigoma Vijijini, mara zote umeme unakatika bila hata taarifa na kusababisha hasara kwa wananchi.

Je, ni nini maelekezo ya Serikali katika kutatua changamoto hiyo ili kupunguza hasara kwa wananchi. (Makofi)

Name

Stephen Lujwahuka Byabato

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bukoba Mjini

Answer

NAIBU WAZIRI WA NISHATI: Mheshimiwa Spika, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Sylvia Sigula, Mbunge wa Viti Maalum, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, Mkoa wa Kigoma ni mmojawapo ya Mikoa ambayo haijafikiwa na gridi ya Taifa, lakini ziko njia tatu zinazopeleka umeme wa gridi ya Taifa katika Mkoa wa Kigoma na mojawapo ilielekezwa na Kiongozi wa Kitaifa Mheshimiwa Makamu wa Rais, kwamba ifikapo Oktoba mwaka huu iwe imekamilika ambayo ni ya kutoka Tabora kupita Uhuru - Nguluka kwenda mpaka Kidahwe.

Mheshimiwa Spika, kazi hiyo inaendelea kufanyika na tunataratijia kabla mwaka huu haujaisha kazi hiyo itakuwa imeisha, tunatarajia itaweza kuweka mazingira mazuri ya upatikanaji wa umeme katika Mkoa wetu wa Kigoma badala ya kutumia zile mashine za mafuta ambazo ziko kwa sasa na zinashindwa kuzalisha umeme wa kutosha kwa wananchi wetu wa Kigoma na hivyo mambo yatakuwa mazuri kabisa.