Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 7 Sitting 9 Energy and Minerals Wizara ya Nishat 79 2022-04-20

Name

Jackson Gedion Kiswaga

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kalenga

Primary Question

MHE. JACKSON G. KISWAGA aliuliza: -

Je, ni lini Serikali itapeleka transfoma yenye uwezo mkubwa wa njia tatu katika Kijiji cha Nyamihuu Kata ya Nzihi Jimboni Kalenga?

Name

Stephen Lujwahuka Byabato

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bukoba Mjini

Answer

NAIBU WAZIRI WA NISHATI alijibu: -

Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Mheshimiwa Waziri wa Nishati naomba kujibu swali la Mheshimiwa Jackson Kiswaga, Mbunge wa Kalenga kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, Kijiji cha Nyamihuu ni miongoni mwa vijiji vilivyopata huduma ya umeme kupitia miradi ya usambazaji wa umeme vijijini awamu ya kwanza (REA I) na kufungiwa transfoma ya KVA 100. Huduma ya umeme katika kijiji hiki imesambazwa katika vitongoji nane kati ya vitongoji 12. Vitongoji vinne vilivyobaki vimewekwa kwenye mpango wa kusambaza umeme jazilizi unaotarajiwa kutekelezwa na Wakala wa Nishati Vijijini (REA) katika mwaka wa fedha 2022/ 2023.

Mheshimiwa Spika, hata hivyo, katika bajeti ya mwaka 2022/2023, Serikali imepanga kuongeza transfoma ya pili yenye uwezo wa KVA 100 katika kitongoji cha Wilolesi katika kijiji cha Nyamihuu ili kupunguzia mzigo wa transfoma iliyopo kuhudumia kijiji chote.