Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Margaret Simwanza Sitta

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Urambo

Primary Question

MHE. MARGARET S. SITTA aliuliza: - Je, Serikali ina taarifa gani juu ya Madini yanayopatikana Wilaya ya Urambo na lini itawasaidia Wananchi ili wanufaike na Madini hayo?

Supplementary Question 1

MHE. MARGARET S. SITTA: Mheshimiwa Spika, ahsante. Namshukuru Naibu Waziri kwa majibu yake lakini naomba atoe kauli hapa kwamba Je, baada ya utafiti kukamilika inawahakikishiaje wananchi wa Urambo kwamba wachimbaji wadogo wadogo nao watapa vitalu ili wanufaike na madini yao. (Makofi)

Name

Dr. Stephen Lemomo Kiruswa Mamasita

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Longido

Answer

NAIBU WAZIRI WA MADINI: Mheshimiwa Spika, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Margaret Sitta kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, tumepewa dhamana na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mama Samia Suluhu Hassan, kuhakikisha kwamba tafiti za madini zinapokuwa zimekamilika na maeneo yenye madini yamepatikana tunahakikisha kwamba yametengwa maeneo kwa ajili ya wachimbaji wadogo.

Mheshimiwa Spika, ninapenda kumpongeza Mheshimiwa Mama Sitta kwa sababu amekuwa ni mpambaji mkubwa kuhakikisha kwamba wananchi wa Jimbo la Urambo hawaachwi nyuma katika kuwekeza kwenye biashara ya madini.

Mheshimiwa Spika, kwa ajili hiyo basi nitumie fursa hii kutoa wito kwa Mikoa yetu yote ya kimadini na wilaya zake, tafiti za madini zinapokamilika na maeneo yenye madini yanapokuwa yamepatikana kuhakikisha kwamba wanayatenga maeneo mahsusi kwa ajili ya wachimbaji wadogo na wawape kipaumbele wale ambao madini haya yamepatikana kwenye maeneo yao.(Makofi)

Name

Ritta Enespher Kabati

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. MARGARET S. SITTA aliuliza: - Je, Serikali ina taarifa gani juu ya Madini yanayopatikana Wilaya ya Urambo na lini itawasaidia Wananchi ili wanufaike na Madini hayo?

Supplementary Question 2

MHE. DKT. RITTA E. KABATI: Mheshimiwa Spika, ahsante kwa kunipa nafasi niulize swali dogo la nyongeza.

Je, ni lini Mheshimiwa Waziri atakuja katika Mkoa wetu wa Iringa katika machimbo ya Nyakavangara, Kata ya Malengamakali, Jimbo la Ismani ili aje aone changamoto kubwa za wachimbaji wadogo wadogo pamoja na uwezeshaji? (Makofi)

Name

Dr. Stephen Lemomo Kiruswa Mamasita

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Longido

Answer

NAIBU WAZIRI WA MADINI: Mheshimiwa Spika, napenda kumjibu Mheshimiwa Mbunge kwamba Wizara ya Madini kupitia taasisi zetu za Tume ya Madini, GST na STAMICO tumeweka mkakati kabambe wa kuzungukia nchi nzima kuwajengea uwezo wachimbaji wadogo, kutatua kero zao na kuhakikisha kwamba wanafuata sheria, kanuni na taratibu katika kujipatia maeneo ya kuchimba madini. Hatukuishia hapo tumehakikisha kwamba katika maeneo yote yenye machimbo tunaanzisha masoko ya madini na vituo vya kununulia na kuuzia madini.