Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Deus Clement Sangu

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kwela

Primary Question

MHE. DEUS C. SANGU aliuliza: - Je, ni lini Serikali itajenga walau KM Tatu za barabara ya lami katika Mji wa Laela - Sumbawanga ambao hauna barabara ya lami?

Supplementary Question 1

MHE. DEUS C. SANGU: Mheshimiwa Spika, nakushukuru sana kwa kunipa nafasi hii kuuliza maswali mawili madogo ya nyongeza.

Swali la Kwanza; kwa kuwa, Rais wa Awamu ya Tano Dokta John Pombe Magufuli Hayati, alipotembelea eneo la Kaengesi aliahidi ujenzi wa kilomita Saba za lami kutoka Kaengesa junction mpaka Chitete. Je, ni lini Serikali itapeleka fedha kuanza ujenzi wa barabara hiyo ya lami ambao usanifu na utambuzi wa barabara hiyo umekamilika?

Swali la pili; kwa kuwa, Jimbo langu la Kwela lina Miji mingi midogo, ukianza Mji wa Laela, Mpuyu, Kaengesa, Mji Mdogo wa Muze, Ilemba na Kilyamatuni, Miji hiyo ina barabara za mitaa ambazo hazijatambuliwa bado.

Je, Serikali mna mpango gani wa kuzitambua hizo barabara ili ziweze ku-qualify kupata bajeti kutoka Serikalini?

Name

David Ernest Silinde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tunduma

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DAVID E. SILINDE): Mheshimiwa Spika, naomba kujibu maswali madogo mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Deus Clement Sangu Mbunge wa Jimbo la Kwela kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, ahadi zote za Viongozi Wakuu wa nchi yetu ambazo zimeainishwa zote zipo katika mipango yetu ikiwemo barabara ambayo Mheshimiwa Mbunge ameainisha ya kilomita Saba ambayo Hayati Dokta John Pombe Joseph Magufuli Rais wa Awamu ya Tano alitoa. Kwa hiyo, ipo katika mipango yetu na tunatafuta fedha ili utekelezaji wake uanze.

Mheshimiwa Spika, kuhusu suala la barabara ili ziweze kutambuliwa jambo hilo nimhakikishie tu Mheshimiwa Mbunge kwamba kwa kuwa Miji hiyo inakuwa kwa kasi na bahati nzuri ni maeneo ambayo hata mimi mwenyewe nayafahamu, basi nikuahidi tu kwamba tutatuma wataalamu wetu ili waweze kuzitambua na kuzisajili ili sasa zianze kupatiwa huduma. Ahsante sana.